Site icon A24TV News

TANZANIA YAOMBA KUCHAGULIWA KUWA MJUMBE WA BARAZA TENDAJI LA ITU

Na Mwandishi wa A24Tv

Katibu Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Duniani Bw. Houlin Zhao akiwahutubia washiriki wa Mkutano Mkuu wa Maendeleo ya Mawasiliano Duniani (ITU-WTDC-2022) katika dhifa fupi ya chakula cha mchana, iliyolenga kuendeleza ushirikiano na wadau wa mawasiliano, pembezoni mwa Mkutano Mkuu wa Maendeleo ya Mawasiliano Duniani wa Shirika la Mawasiliano Duniani (ITU-WTDC-2022), tarehe 14 Juni, 2022, jijini Kigali- Rwanda.

Tanzania imetumia fursa hiyo kuomba uungwaji mkono ili kuchaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza-Tendaji la ITU kwenye Mkutano Mkuu wa Shirika hilo unaotarajiwa kufanyika Septemba 2022 jijini Bucharest, Romania.