Site icon A24TV News

RAIS DK.MWINYI AKUTANA NA NAIBU KAMISHNA WA HAKI ZA BINADAMU

Na Mosses Mashala .

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amekutana na Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu, Nadal Al-Nashif na ujumbe wake Ikulu Zanzibar tarehe: 9 Machi 2024.

Aidha Rais Dk.Mwinyi amesema Zanzibar kuimairisha ushirikiano katika kujenga uwezo Taasisi za kisheria hususani utekelezaji wa sheria, Mahakama na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka .

Naye Naibu Kamishna Nadal Al-Nashif amesema wataisaidia Zanzibar katika kuwajengea uwezo hususani Taasisi za kisheria.

Vilevile katika mazungumzo yao wamezungumzia nafasi ya Vyombo vya habari, huduma za maendeleo ya kijamii, utalii, Serikali ya Umoja wa Kitaifa, na uwezeshaji wa Wanawake na Vijana .

Mwisho .