ROSE NJILO AJITOSA UBUNGE JIMBO LA NGORONGORO NINA UWEZO WA KUONGOZA JIMBO .
Geofrey Stephen
Makada wa Chama Chamapinduzi Ccm Wilayani NgoroNgoro Mkoani Arusha wajitosa kugombea nafasi za ubunge .
Katika Makada wa Ccm walio jitosa nafazi hizo ni pamoja na Mwanarakati wa haki za wanawake na watoto Rose Njilo wa Shirika la Memute Women Organization.
Zoezi la Utoaji fomu za wagombea Ubunge wa Jimbo la Ngorongoro umaeanza rasmi leo huku likisimamiwa na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya chini ya Mwenyekiti wake Ndg.Augustino Yessaya Simon Mbogo. Mkurugenzi wa Uchaguzi amewataka wagombea kuepuka vitendo vya rushwa ,kukusanya wajumbe na kuchafuana.