Na Mwandishi wa A24tv Handeni Tanga .
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais -TAMISEMI
anayeshughulikia Afya, Prof. Tumaini Nagu, ameongoza kikao kazi kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Handeni, kwa lengo la kupokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa miradi ya afya katika Halmashauri zote mbiliza Wilaya hiyo.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, Wakurugenzi wa Halmashauri ya Mii Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, pamoja na Maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Katika kikao hicho, Prof. Nagu alipokea taarifa za maendeleo ya miradi ya ujenzi wa miundombinu ya afya, hali ya upatikanaji wa rasilimali watu, hali ya vifaa tiba, na utekelezaji wa shughuli za afya za msingi. Alieleza kuwa lengo la Serikali kupitia TAMISEMI ni kuhakikisha kila mtanzania anapata huduma bora za afya kwa wakati, na kwa ubora unaokubalika.
Mhe. Nyamwese alieleza kuwa Wilaya ya Handeni inatekeleza kwa bidii maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha huduma za afya, na akaeleza kuwa ushirikiano kati ya viongozi wa kisiasa, wataalamu, na wadau umechangia mafanikio yaliyopo.
Mwisho .