Na Bahati Hai,
Kukamilika kwa ujenzi wa Shule mpya ya msingi Sadala iliyopo kitongoji cha Matowo Wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, itasaidia kupunguza msongamano katika shule ya Msingi msamadi yenye watoto zaidi ya 1000
Mradi huu umetekelezwa kwa gharama ya zaidi ya sh,300 milioni kutoka Serikali kuu ,uku nguvu za Wananchi wakiwekeza katika kuchimba msingi wa vyumba vya madarasa.
Haya yamesemwa na Diwani wa kata ya masama kusini Sedrick Pangani,wakati wa zoezi la upandaji miti katika Shule hiyo,ikiwa sambamba na maadhimisho ya Karume day
Akizungumza leo April 7 ,2025 na Wananchi pamoja na Viongozi wengine walioshiki katika zoezi hilo, ameshukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kutoa fedha za ujenzi huo na kuondoa masongamano uliokuwepo kwani imekuwa kero kwa wanafunzi
“kweli shule ya msingi msamadi ina watoto zaidi ya 1000 ni wengi na kusababisha msongamano makubwa ambao umekuwa kero kwa wanafunzi kwa kushindwa kusoma vizuri jambo ambalo litasababisha wanafunzi kutokufanya vizuri kwenye masomo yao “amesema Pangani
Amesema mbali na msongamano kumekuwa na changamoto ya wanafunzi kugongwa na magari wakati wakivuka barabara wanaelekea shuleni kwani imewasababishia matatizo ikiwamo ya kugongwa na kufariki, hivyo kukamilika kwa ujenzi huu itasaidia kuondoka tatizo hilo.
Pangani amesema kijografia katika Kijijii cha Sadala kuna mkusanyiko mkubwa wa watu ,hivyo kuwa na shule moja katika eneo hilo ya msingi msamadi ni kitu kisicho wezekana
Ndiyo sababu ya ujenzi wa shule mpya, hatuna budi kutoa shukrani kwa Rais Samia Suluhuu Hassani kwa kuona umuhimu kwa watu wa Sadala kwa kutumia fedha ili shule ikamilike na watoto wasome bila kuwa na usumbufu wowote ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao
Aziza Tarimo mmoja ya Wananchi wa maeneo hayo ya kitongoji cha Matowo amesema kukamika kwa shule hiyo,itawasaidia watoto kupungua umbali mrefu kufuata masomo , Sadala mjini ni mbali Bomang’ombe ni mbali ,tunaishukuru Serikali kwa ujenzi huu
Awali Issa Sadiki Mwenyekiti wa Kitongoji hicho, amesema wanewaka faini ya sh,50,000 kwa ngo’mbe mmoja atakayeingia na kuharibu miti iliyopandwa na faini ya sh,5000 Kwa mbuzi,hii ni kulinda mazingira.
Amesema mtu yeyote atakaye kamata mifugo ikiharibu miti kwenye shule hiyo atapata sh,10,000 kwa Kila ngo’mbe mmoja hiii yote ni kulinda miti iliyopandwa,mwaka jana tulipanda miti 10,000 yote ililiwa na mifugo
Mwisho