Author: Geofrey Stephen

Na Doreen Aloyce, Dodoma. Meneja Mawasiliano Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Bi. Subira Kaswaga, amezitaka Taasisi za Umma nchini kuendesha vikao kidijitali kwa kutumia mfumo wa e-Mikutano ili kupunguza gharama za uendeshaji wa vikao. Kaswaga ametoa rai , alipofanya mazungumzo na mwandishi wetu ofisini kwake jijini Dodoma kuhusu faida zitokanazo na mfumo wa e-Mikutano. Amebainisha kuwa, mfumo wa e-Mikutano unawawezesha watumishi wa Taasisi za umma kufanya vikao kidijitali mahali walipo bila kulazimika kukutana mahali pamoja na hivyo kusaidia kupunguza gharama za uandaaji na uendeshaji wa vikao. “Mfumo huu wa e-Mikutano unazisaidia taasisi za umma kupunguza gharama za uendeshaji wa vikao,…

Read More

Na Geofrey Stephen Lushoto Miradi 17 yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 2 inatarajiwa kuzinduliwa na Mbio za Mwenge Kitaifa katika wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga na Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuwasili katika wilaya hiyo kesho na utazunguka katika Wilaya hiyo kwa umbali wa km 304. Akizungumza na Waandishi wa Habari Leo ofisini kwake,Mkuu wa Wilaya ya Lushoto,Kalisti Lazaro alisema kuwa Mwenge utapokelewa Lushoto katika Kijiji Cha Samata kilichopo Halmashauri ya Bumbuli na utazungushwa katika Halmashauri hiyo kwa umbali wa km 122 na miradi 9 itazinduliwa yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 779. Kalisti Lazaro akizungumza na Vyombo…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha Watetezi wa Haki za Binadamu nchini Tanzania wameiomba serikali kusitisha zoezi la kubadili vijiji 14 na kuwa pori tengefu la Pallolet ili kulinda, kuhifadhi na kuendeleza haki za binadamu kwa wananchi wa Tarafa ya Loliondo na sehemu ya Tarafa ya Sale. Ombi hili la watetezi wa haki za binadamu limekuja baada ya watetezi hao kufanya ziara mwezi Mei katika vijiji vya Msomera wilayani Handeni mkoani Tanga, Tarafa ya Loliondo na Sale wilayani Ngorongoro mkoani Arusha ili kuangalia hali ya haki za binadamu katika maeneo hayo. Odero Charles Odero, Mkurugenzi CILAO akizungumza na waandishi wa habari ofisini…

Read More

Na Pamela Mollel,Arusha Jamii imeaswa kuzingatia maadili na kuacha vitendo viovu na kufanya yale yanayo mpendeza Mungu ikiwemo kufanya kazi kwa bidii na uaminifu katika nafasi tunazopewa ili nchi iweze kuwa na maendeleo na kupiga hatua kiuchumi. Hayo yameelezwa na Baba Askofu Dkt. Solomoni Jacob Massangwa ambae pia ni Mkuu wa Dayosisi ya kaskazini kati kanisa la kilutheri Tanzania katika ibada ya kumstaafisha parishworker wa jimbo la Arusha Mashariki Bi. Rebeca Christopher Mungure ambae amekuwa kwenye utumishi takribani miaka 40. Askofu Dkt. Solomoni Masangwa alisema kuwa jamii kwa ujumla inapaswa kuiga mfano mzuri kutoka kwa Parishworker huyo aliyejitoa kumtumikia Mungu…

Read More

Na Mwandishi wetu Arusha Mzee Edward Mollel{65} Mkazi wa Sanawari Jijini Arusha ameliomba jeshi la Polisi Mkoani Arusha kufanya kila linalowezekana kumkabidhi maiti ya mwanaye,Faraja Mollel{8} aliyechinjwa kinyama na watu watatu wanaojulikana ambao walitumwa na Mfanyabiashara Maarufu ya Madini ya Tanzanite Jijini Arusha kwa manufaa yake vinginevyo atamwona Rais Dk Samia Suluhu Hassan ili aweze kumsaidie. Mollel alisema waliofanya tukio hilo wote wamekamatwa na Polisi Arusha ni pamoja na Amina Poul maarufu kwa jina la Ester ambaye ni mpangaji wake  katika nyumba anazomiliki eneo la nyumbani kwake Sanawari ,Mganga wa kienyeji mkazi wa Babati aliyemtaja kwa jina la John Mtai…

Read More