Author: Geofrey Stephen

Na Geofrey Stephen Arusha Mapema leo akifungua mkutano wa senima kwa wana hisa Makamu wa Rais , Dkt Philip Mpango  amezitaka Taasisi za  fedha na mabenki nchini  kutoa mikopo ya riba nafuu kwa makundi maalum na  mbalimbali wakiwemo wachimbaji wadogo wa madini,wavuvi, wakulima na wafugaji  ili waweze kupiga hatua kujenga uchumi wa taifa.   Ameyasema hayo leo jijini Arusha wakati akifungua  mkutano kwa wanahisa wa benki ya CRDB unaofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Aicc jijini Arusha. Alisema kuwa,taasisi n noyingi za fedha zimekuwa zikitoa mikopo ya riba kwa asilimia 9 ,hivyo aliomba kupunguza zaidi chini ya asilimia 9 ili kuwapa…

Read More

Na Geofrey Stephen Stephen Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa waheshimiwa mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani kushirikiana na makampuni ya mawakala ya utalii katika nchi husika kuwaleta watalii nchini ili kuifikia azma ya kuwaleta watalii milioni tano ifikapo 2025 na kukuza uchumi wa nchi. Mhe. Mchengerwa ametoa kauli hiyo leo Mei 18, 2023 wakati akisoma hotuba yake kwenye mkutano maalum wa kibiashara baina ya makampuni makubwa duniani ya watalii kutoka nchini China na wadau wa utalii nchini jijini Arusha alipokuwa ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Anderson Mutatembwa. Amempongeza Balozi wa…

Read More

Doreen Aloyce, Dodoma SERIKALI imesema Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) licha ya kufanya vizuri limeendelea kujipambanua katika utoaji wa huduma zake za Mawasiliano iliyopelekea kufikisha huduma za mawasiliano Kilele cha Mlima Kilimanjaro. Hayo yamebainishwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Ackson wakati alipotembelea na Kukagua Banda la Shirika hilo lililopo katika Maonesho yaliyoandalaliwa na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ,kwa taasisi zilizopo Chini yake yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma. Dkt.Tulia amesema kuwa TTCL mbali na ubunifu wao wamekuwa chachu kuifungua nchi kidijitali jambo ambalo limesaidia kuchochea maendeleo ya Mtu…

Read More

Na Doreen Aloyce, Dodoma Mbunge wa Jimbo la Pangawe Haji Amri Haji amesema kuwa ili Taifa liweze kusonga mbele kiuchumi kunapaswa kuwa na lugha ya kiswahili huku akiitaka Sekta ya Elimu kubadilka katika ufundishaji wa lugha . Mbunge Haji ametoa kauli hiyo Katika Viwanja vya Bunge wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari juu ya Bajeti ya Elimu kwa mwaka 2023/2024 ambayo imepitishwa na wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha amesema kuwa nchi nyingi za ulaya zilizoendelea hususani nchi ya Lashia na China zimekuwa zikitumia lugha zao kwa sababu ya mfumo wa kibiashara na mfumo wa…

Read More

Matukio katika hafla ya kukabithi piki piki katika kituo cha diplomatic polisi station cha Jijini Arusha na Waziri wa maliasili na utalii Mh Mohamed Mchengerwa kwa jeshi la polisi kitengo cha utalii Waziri wa maliasili na utalii amekabidhi pikipiki 15 na kutoa ujumbe zitumike katika kazi za serikali ususani kukuza utalii kwa jiji la arusha na viunga vyake Waziri wa maliasili na utalii Mohamed Mchengerwa akizungumza katika hafla ya kukabidhi piki piki kwa jeshi la polisi mkoani arusha kitengo cha dilpomatic cha utalii  Katika hafla hiyo Mh Waziri amelitaka jeshi la polisi kitengo cha utalii kutumia piki piki hizo katika…

Read More

Na Richard Mrusha Bukombe WAZIRI wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Dkt. Doto Biteko ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuendelea kuboresha maslahi ya watumishi na kuweka mazingira wezeshi mahala pa kazi ikiwemo kwa wauguzi. Amesema Bukombe tunatambua mchango mkubwa unaotolewa na wauguzi katika kuimarisha Afya zetu, tunatakiwa kuwalinda na kuendelea kuwapa ushirikiano uliyobora kwa Sababu hao nao ni binadamu ili kuhakikisha wanafanya kazi yao kwa weledi. Ameyasema hayo Mei 17, 2023 Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Dkt. Doto Biteko wakati akiongea na Watumishi wa Idara ya…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha Kwa mwaka huu wa 2023 Zaidi ya nchi 30 kutoka Duniani na makampuni zaidi ya 300 zinatarajia kushiriki maonyesho ya Karibu kill fair viwanja vya Magereza kisongo jijini Arusha. Akizungumza na Vyombo vya habati  Mkurugenzi mtendaji  wa kill fair promotion limited Dominic Shoo  amesema kuwa maonyesho  ya  karibu Kili fair inauza Tanzania kwasababu ya kutembelea na kutafuta masoko nchi zingine duniani Ili waweze kuonana na watanzania. Shoo amesema kuwa ongezeko la utalii nchini Tanzania limechangiwa zaidi na kampuni ya karibu kill fair ambapo amesema kmataifa hayo yatakayoshiriki yanatarajia kua na lengo la kuona Tanzania ina nini…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha. BENKI ya CRDB imeikabidhi Wilaya ya  Arusha Madarasa ya kisasa mawili vyenye thamani ya sh,milioni 42 katika shule ya Sekondari Kilimaji ya Jijini Arusha hiliyopo katika kata ya Moshono yakabidhiwa katika Mkoa wa Arusha  ikiwa ni jitihada za kuunga mkono serikali katika kuboresha miundo ya elimu Nchini. Akiongea katika hafla hiyo ikiwa ni sehemu ya kuelekea mkutano mkuu wa 28 wa wanahisa wa CRDB, iliyofanyika katika shule hiyo, iliyopo kata ya Moshono,jijini Arusha. Mkurugenzi mtendaji wa benki  ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema msaada huo umetokana na sera ya benki hiyo kurudisha asilimia moja ya mapato…

Read More