Author: Geofrey Stephen

Na Geofrey Stephen Arusha kesi ya kulazimishwa kupotea Mzee Oriais Oleng’iyo mkazi wa  Ololosokwani tarafa ya Loliondo itajulikana Mei 10,2023. Mahakama Kuu ya Tanzania,Masijala ya  Arusha, Leo imesikiliza maombi madogo yaliyoletwa na Ndoloi Oriais ambaye kupitia Mawakili wake imewataka  wajibu maombi kwa ujumla wao kumleta, kumuachilia au kusema popote alipo Mzee Oriais Pasilange Oleng’iyo(85). Wajibu maombi ni pamoja na Kamanda wa jeshi la polisi (RPC), Mkuu mkoa wa Arusha, Mkuu wa wilaya na OCD Ngorongoro, Mkuu wa jeshi la polisi(IGP) na Mwanasheria Mkuu wa serikali. Mbele ya Jaji Mohamed  Gwae,Wakili wa mleta maombi, Saimon Mbwabwo aliieleza kuwa Juni 9,2022 huko…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv. Kaimu Mkurugenzi Kitengo cha Mazingira ya Biashara cha Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Bw. Baraka Aligaesha amewashauri Maafisa Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kutangaza na kielimisha umma kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji nchini (MKUMBI) . Bw. Baraka ameyasema hayo wakati akiwasilisha mada kuhusu utekelezaji wa MKUMBI na mafanikio yake katika Kikao Kazi cha 18 cha Maafisa Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) Machi 29, 2023 JNICC jijini Dar es Salaam. Akiongea na Maafisa hao, amesema ni jukumu la kila Afisa Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kutangaza na kuelimisha umma kuhusu maboresho yanayotokea…

Read More

Na Doreen Aloyce, Dodoma SHIRIKA La Umeme Tanzania (TANESCO), limezindua Programu ya Mpango wa miaka minne wa jinsia wenye lengo la kutatua changamoto za wanawake katika maeneo yao ikiwemo vitendo vya unyanyasaji. Akizindua program hiyo Naibu Waziri wa Nishati Stephen Byabato amesema mradi huo unalenga kutengeneza sera za shirika na kujenga uwezo kuhusu masuala ya unyanyasaji wa kijinsia. Amesema mradi huo, utasaidia kuwepo kwa taarifa sahihi za unyanyasaji wa kijinsia katika shirika, kuruhusu fursa ya ukuzaji taaluma kwa wafanyakazi wanawake na kuongeza mafunzo kwa vitendo kwa wafanyakazi wanawake waliopo kazini. “Mradi huu unatekelezwa na TANESCO lengo ni kuhakikisha watumishi wanaofanya…

Read More

Na Doreen Aloyce, Dodoma. Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi ameridhishwa maendeleo ya miradi ya ujenzi inayosimamiwa na Ofisi hiyo ambapo amesema kukamilika kwake kutawezesha watumishi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi (wa kwanza) akikagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali linalojengwa Kisasa, Jijiji Dodoma alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maeneo ya miradi ya ujenzi iliyopo chini ya Ofisi hiyo. Dkt. Yonazi ameyasema hayo alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa maeneo…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv . Kilele cha Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu kinatarajia kufanyika Aprili 13, 2023 Jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na waandishi mahiri kutoka nchi mbalimbali duniani. Hayo yamesemwa leo Machi 29, 2023 kisiwani Zanzibar na Prof. Adolf Mkenda, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari ambapo amesema tuzo hizo zitakuwa zikifanyika kila mwaka tarehe 13 Aprili ikiwa ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere. Waziri Mkenda ametaja malengo makuu ya tuzo hizo kuwa ni kukuza uandishi bunifu, kukuza usomaji,…

Read More