Na Doreen Aloyce, Dodoma IMEELEZWA kuwa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu(TPHPA) kumekuwa na vikwazo katika kukabiliana na wadudu waharibifu wa mimea nchini kutokana na udanganyifu wa baadhi ya wauzaji wa viuatilifu. Hayo yameelezwa a jijini Dodoma na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya mimea na viuatilifu (TPHPA) Dkt. Joseph Ndunguru wakati akieleze mafanikio na utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo. Hali hiyo ni kutokana na uelewa mdogo wa wakulima na wadau wengine juu ya matumizi sahihi ya viuatilifu pamoja na kuwepo kwa wauzaji wa viuatilifu na mazao ya mimea wasio waaminifu na kusababisha kuendelea kuwepo kwa…
Author: Geofrey Stephen
Karibu Arusha 24 Tv leo Tarehe 2 Mwezi Marchi kutazama kilicho Andikwa katika magazeti ya leo ya Tanzania Hii ni A24Tv .
Waziri wa uchukuzi na ujenzi Profesa Makame Mbarawa ameridhishwa na ujenzi wa wakala wa majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Arusha. Akizungumza mara baada kutembelea jengo Hilo katika ziara yake Mkoani Arusha amesema jengo Hilo libaendana na thamani ya fedha zilizotolewa ikiwemo Bilioni5.2 ambapo mpaka kukamilika litagharimu Kiasi Cha fedha za Kitanzania Bilioni 5 . Kwa upande wake kaimu meneja TBA Mhandisi Juma Dandi amesema kuwa jengo hilo ambaloo ni kitega uchumi kutoka katika mamlaka hiyo ambapo mpangaji katika nyuma hiyo atapaswa kulipa Kwa wakati. Alisema kuwa jengo Hilo litatumia mfumo wa Kitasa Janja Ili kuwabaini wadaiwa sugu Kwa hii itasaidia…
CHAMA cha Mapinduzi CCM kupitia jumuiya ya wazazi mkoani hapa, kimejitosa kupambana na ukatili wa kijinsia wilayani Arumeru huku kikipinga adhabu ya fimbo 70 kwa vijana wanaoenda kinyume na maadili. Pamoja na hatua ya wazee wa ukoo (Washiri)wilayani humo kutumia mila zao kuwarekebisha vijana kwa kuwachapa fimbo 70 ,chama hicho kimesema ipo haja kutazamwa upya umuhimu wa kuendelea na mila hizo ,kwani zinachochea ukatili Katibu wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Arusha Deogratias Nakey ameyasema hayo wilayani humo, alipokuwa akiongea na wanachama wa ccm wakati kamati ya utekelezaji ya umoja wa wazazi mkoa wa Arusha,ilipotembelea wilaya hiyo kukakugua uhai na…
Katika Kikao cha Umoja wa Waijilisti Arusha Mwenyekiti Baraka amesema anatamani aone mafanikio makubwa yanafikiwa na wainjilisti wenzake kuona wanapata bima za afya wote kuondokana na garama kubwa wanazo lipia pindi wanapo pata matatizo ya kiafya . Akizungumza na A24Tv Mwenyekiti Baraka Mollel amesema pia wanaomba kuboroshewa posho na pia zilipwe kutokana na watumishi mazingira wanayo fanyia kazi pamoja na kupata kwa wakati . Katika umoja huo wainjilisti wameeleza changamoto kadhaa wanazo pitia nakuomba kufanyiwa utatuzi kwa lengo la kuendelea kufanya kazi zao kwa umakini zaidi , Wameeleza changamoto zao ni pamoja na wainjilisti wenzao kukataa umoja huo baadhi ya…
Karibu Arusha 24Tv leo tarehe 1,March 2023 kutazama kilicho Andikwa katika Magazeti ya leo ya Tanzania mbele na nyuma Hii ni A24Tv .
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Carolyne Nombo amewataka watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa umahiri, weledi na ubunifu ili malengo ya sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaweze kufikiwa. Prof. Nombo ametoa wito huo jijini Dodoma wakati wa mapokezi yake na Naibu Katibu Mkuu Dkt. Franklin Rwezimula baada ya kuteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo amesema Wizara hiyo imepewa majukumu makubwa ya kuhakikisha elimu inayotolewa kwa Watanzania inakuwa bora na kuimarisha Sekta ya Sayansi na Teknolojia. Ameongeza hivi sasa Wizara ipo katika hatua za mwisho za…
Na Geofrey Stephen Arusha Katika kutimiza Miaka 60 ya KKKT na Jubilee ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Kanisa Dayosisi ya kaskazini kati umoja wa wainjilisti wakutana na Askofu wao Doctar Solomon Masangwa . Askofu wa KKKT dayosisi ya kaskazini Kati Ask.Dkt Solomon Masangwa amewataka watumishi wa Mungu kusaidiana ili kuongeza thamani katika huduma walizo nazo wakianza na familia zao Askofu Solomon Masangwa Akifungua Mkutano wa Umoja wa Wanjilisti kandaya Kaskazini Ameyasema hayo leo katika mkutano na Baba askofu na wainjilisti wote wa dayosisi ya kaskazini kati uliofanyika usharika wa Ilkiranyi jijini Arusha Askofu Amesema kuwa kusaidiana kunaanzia nyumbani katika…
Na Geofrey Stephen Arusha Wadau wa Tehama mkoani Arusha wametakiwa kutoa ushirikiano wa kutosha ili.kufanikisha uwepo wa kituo cha ubunifu wa Tehama kinachotarajiwa kuanzishwa mkoani Arusha hivi karibuni. Akizungumza katika ufunguzi huo leo jijini Arusha Kaimu Katibu Tawala msaidizi Daniel Loiruck amesema kuwa uwepo wa kituo hicho utaongeza chachu kubwa kwa vijana katika kuendeleza bunifu zao kupitia Tehama na kujulikana kimataifa zaidi. Amesema kuwa ,uwepo wa vituo hivyo utasaidia sana kuibua vituo vya ubunifu kwa vijana kutoka katika halmashauri Ili kufungua fursa zakiuchumi kupitia Tehama. Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Tehama Dr Nkundwe mwasaga amesema kutokana na…
Doreen Aloyce, Dodoma. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanapa Dodoma kwa jitihada za kuunga juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan kuutangaza utalii wa ndani hapa nchini ambao umepelekea wananchi kuwa na mwitikio kutembelea vivutio mbalimbali. Kauli hiyo ameitoa jijini Dodoma wakati alipokuwa akiwaaga wadau wa utalii kutoka sehemu mbalimbali wakielekea kutembelea mashamba ya Zabibu kijiji cha Nkulabi kilichopo nje kidogo na mji wa Dodoma ambapo ziara hiyo imeandaliwa na Hifadhi za Tanapa Dodoma kwa kushirikiana na Taasisi ya Dodoma Wine Festival. Senyamule amesema kuwa uongozi wa Tanapa Dodoma wamekuwa kielelezo kutangaza vivutio…