Author: Geofrey Stephen

Na Geofrey Stephen Arusha . Wafanyabiashara katika soko kuu la Arusha wameiomba halmashauri ya jiji la Arusha kuboresha miundo mbinu ya soko hilo kutokana na majengo yake kuchakaa na maduka kuvuja wakati wa mvua na kusababisha kukosa mvuto kwa wateja wakiwemo watalii wanaofika kwa ajili ya kujipatia mahitaji mbalimbali. Miongoni wa kero walizozitaja   ni pamoja na uchakavu wa soko hilo, baadhi ya maeneo kukosa umeme,ukosevu wa vyoo,watu kujisaidia ovyo kwenye vizimba vya biashara,sehemu ya maduka kuvuja wakati wa mvua,Wafanyabiashara kuacha vizimba na kupanga bidhaa zao kiholela ,jambo linalosabahisha wateja walikimbie soko hilo na kwenda masoko mengine. Wakiongea kwenye mkutano…

Read More

By A24 Tv Mtaalii mmoja mwenye asili ya China amefariki dunia na wengine sita wamejeruhiwa baada ya gari la Watalii lenye namba za usajili T603 DCL mali ya Kampuni ya Yonda Africa walilokuwa wanalitumia, kupata ajali likiwa njiani kurudi hotelini kilomita moja kutoka Lobo Wildlife Lodge katika Hifadhi ya Taifa Serengeti. Taarifa iliyotolewa usiku huu na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) imesema “Majira ya saa 10 jioni July 28,2024 gari la Watalii lenye namba za usajili T603 DCL mali ya Kampuni ya Yonda Africa lilipata ajali likiwa njiani kurudi hotelini kilomita moja kutoka Lobo Wildlife Lodge katika Hifadhi…

Read More

Na Mwandishi Wetu-DODOMA Waziri wa Madini Mhe Anthony Peter Mavunde amepiga marufuku kwa wamiliki wa Leseni za uchimbaji mdogo wa Madini kuingiza wageni kutoka nje ya Nchi kwenye leseni zao bila kuwa na mikataba au makubaliano yaliyopitishwa kwa mujibu wa Sheria. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Jijini Dodoma July 28,2024 wakati akizungumza na Wanahabari kuhusu Mwendendo wa makusanyo ya maduhuri yatokanayo na rasilimali madini Nchini kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 na Katazo la Wageni kuungia kwenye PMLs bila kuwa na makubaliano ya msaada wa kiufundi(TSA). Na kupiga marufuku kwa Wageni wenye leseni kubwa za biashara ya madini hususan…

Read More

Na Richard Mrusha MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)iliyo chini ya Wizara ya Afya, imetoa taarifa kwa Umma ufafanuzi kuhusu uvumi juu ya Dawa ya Paracetamol inayodaiwa kubabua ngozi. Kwa mujibu wa taarifa hiyo kwa Umma liyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, DKT. Adam Fimbo Imebainisha kuwa, imebaini uwepo wa taarifa inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu uwepo wa dawa aina ya Paracetamol ambayo imeandikwa P 500 na kudaiwa kubabua ngozi kama inavyooneshwa (pichani). Akinukuu taarifa hiyo inayosambazwa mitandaoni: “Dawa hiyo inadaiwa kuwa ni ‘’paracetamol mpya nyeupe sana na inayong’aa, madaktari wanashauri kuwa ina virusi vya “Machupo”, inayochukuliwa kuwa…

Read More

Na Bahati Hai Wananchi Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro wanaalikwa kwenye Uzinduzi wa Mashindano ya West CHAMPIONS LEAGUE yatakayo anzakutimua vumbi Juma pili Julay 28 mwaka huu,Saa saba Mchana katika Uwanja wa Kilimahewa Matadi West Kilimanjaro Hayo yamesemwa leo na ELI Pius mwasisi wa mashindano hayo mwaka wa tatu ,ambapo amesema ya uzinduzi itakuwa kati ya Zinduka fc na Kware kutoka Wilayani Hai Zinduka FC imerudi Wale Mashabiki wa Zinduka wafike kwa Wingi kujakuiona Zinduka Mpya yenye Nguvu Mpya na Kasi ya 4G BURUDANI KEDEKEDE ZITAKUWEPO .TUTAKUWA NA WASANII WAKUMBWA WATAKAO PAFOMU KWENYE JUKWAA .WASANII KAMA MR VOICE POLELA ,DULLA NATION…

Read More