Author: Geofrey Stephen

Mwandishi wetu,Arusha. Wanafunzi wa shule ya msingi Prestige ya jijini Dar es salaam,wameeleza maajabu ya vivutio vya utalii vilivyopo nchini na kushauri watoto wa shule nyingine kupatiwa nafasi ya kutembelea hifadhi za taifa na maeneo ya vivutio vya utalii. Wakizungumza na waandishi wa habari, wakiwa na kituo cha Utalii cha Cultural Heritage jijini Arusha, baada ya kutembelea Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, hifadhi ya Taifa ya Tarangire na hifadhi ya taifa ya Manyara, wanafunzi hao wameeleza kuona maajabu mengi katika hifadhi hizo. wanafunzi Kenzi Lewanga,Jaden James, Diana Komu ,Illa Munisi na Ebeneza Charles wamesema hakuwahi kuona kama Tanzania imejaliwa kuwa…

Read More

Na Mwandishi wa A24Tv Geita . Kamishna wa Tume ya Madini Janet Lekashingo amewataka watanzania kujitokeza kwenye uwekezaji katika Sekta ya Madini kutokana na kuwepo kwa fursa mbalimbali kwenye mnyoyoro wa madini kuanzia uchimbaji, uchenjuaji, biashara ya madini na utoaji wa huduma kwenye migodi ya madini. Lekashingo ameyasema hayo kupitia kipindi cha Jambo Tanzania kilichorushwa mubashara na kituo cha televisheni cha TBC1 leo tarehe 08 Oktoba, 2022 kwenye Maonesho ya Tano ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini katika Viwanja vya Bombambili mjini Geita. Amesema ili kuhakikisha kila mtanzania ananufaika na Sekta ya Madini, Serikali kupitia Wizara ya Madini imeweka mikakati…

Read More

*Na WyEST – Mwanza Serikali kupitia Wizara ya Elimu. Sayansi na Teknolojia inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa kituo cha umahiri katika sekta ndogo ya ngozi. Kituo hicho kinachojengwa katika Chuo cha Teknolojia cha Dar es Salaam (DIT) kampasi ya Mwanza kinalenga kuimarisha mafunzo ya ujuzi juu ya bidhaa za ngozi yanayotolewa katika kampasi hiyo. Akielezea namna wizara ilivyojipanga katika kukiimarisha kituo hicho mara baada ya ya kukagua utekelezaji wa Mradi huo mwishoni mwa wiki Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema shilingi bilioni 19.6 zimetengwa katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2022/23 kwa…

Read More

Na Mwandishi wa A24Tv Geita Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula akiwa ameambatana na Kamishna wa Tume ya Madini, Janet Lekashingo ametembelea banda la Wizara ya Madini, Tume ya Madini na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kwenye Maonesho ya Tano ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea katika Viwanja vya Bombambili, mjini Geita. Katika Banda la Wizara ya Madini alielezwa kuhusu namna Wizara ya Madini inavyoandaa na kusimamia Sera na Sheria ya Madini pamoja na kanuni zake pamoja na mikakati iliyowekwa katika kuhakikisha watanzania wananufaika na Sekta ya Madini. Katika banda la Tume ya Madini elimu ilitolewa katika…

Read More

Na Geofrey Stephen . Arusha HALMASHAURI ya jiji la Arusha imepokea kiasi cha sh,bilioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 100 vya madarasa katika shule za sekondari za jiji hilo ili ifikapo januari 2023 wanafunzi wote watakaochaguliwa kuingia kidato cha kwanza wawe wamejiunga na shule za sekondari. Hayo yamebainishwa na mkuu wa wilaya ya Arusha,Said Mtanda wakati akiongea na wakuu wa shule za serikali jijini hapa na kutoa siku 75 kuanzia leo , ujenzi wa madarasa hayo uwe umekamilika kwa kiwango na ubora unaotakiwa. Hata hivyo Mtanda alitahadhalisha matumizi mabaya ya fedha hizo na kuwaonya wakuu wa shule watakaoenda…

Read More