Author: Geofrey Stephen

Na mwandishi wetu Ofisi ya Waziri Mkuu yaibuka mshindi wa kwanza kwa banda bora na utoaji bora wa huduma kwa ngazi ya Wizara zilizoshiriki katika maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) jijini Dar es salaam. Akipokea tuzo ya Ofisi hiyo kwa niaba ya Uongozi wa Ofisi, Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi Bw. Condrad Millinga ameshukuru kwa namna ushindani ulivyoenda na kuipa Ofisi ya Waziri Mkuu ushindi wa Kwanza katika maonesho hayo. Amepokea tuzo hiyo kutoka kwa Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Sulemani Jafo hii leo Julai 13, 2024. Maonesho hayo yamefungwa…

Read More

Na Bahati Siha, Waganga wa tiba asili na tiba mbadala Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro,wametakiwa kuwataja watu wanaofanya shughuli hizi bila kuwa na vibali ili Sheria iweze kuchukua mkongo wake Pia kwa wale ambao vibali vyao muda wake unataka kumalizika wametakiwa kuviuisha tena Haya yamesemwa na Mkuu wa Wilayani hiyo Christopher Timbuka,alipokutana na wahudumu hao wa tiba asili katika ukumbi wa Hospitali ya Wilayani hiyo,kwa lengo la kuimarisha ulinzi na usalama katika wilaya hiyo. Akizungumza katika kikao hicho Amewataka wahudumu hao kufanya kazi kwa mujibu na utaratibu unaokubalika na kwa mujibu wa vibali vyao “Kubwa ni kufuata utaratibu zilizopo, nafahamu mratibu…

Read More

Na Richard Mrusha Serikali ya Jamhuri ya Burundi leo tarehe 12 Julai 2024 imezindua ujenzi wa miundombinu katika eneo la Bandari kavu ya Kwala lililoko Mkoani Pwani. Uzinduzi huu unaashiria kuanza rasmi kwa ujenzi wa Uzio Pamoja na miundombinu ya kibandari kwenye eneo la hekari 10 ambalo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) iliikabidhi kwa Serikali ya Jamhuri ya Burundi. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Waziri wa Uchukuzi wa Burundi Mhe.Marie Chantal Nijimbere amesema uendelezaji wa Bandari kavu hii ni kiungo muhimu katika ukuaji wa uchumi wa nchi hizi mbili na uendelezaji wa…

Read More

Na Richard Mrusha Wananchi wametakiwa kutumia mfumo wa e- mrejesho katika kuwasilisha changamoto zao kwa Serikali na kutoa hoja zao ili ziweze kufanyiwa kazi. Rai hiyo imetolewa na Mamlaka ya Serikali e- mrejesho katika mtandao wake wa (eGA) kwa lengo la kushughulikia changamoto za wananchi kwa haraka zaidi. Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la eGA kwenye maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) jijini Dar Dalaam Meneja Mawasiliano wa eGA Subira Kaswaga amesema suala la kujenga mifumo kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi katika utumishi wa umma ni jukumu la eGA huku akisema katika jukumu hilo imejenga…

Read More

Na Richard Mrusha Taasisi ya Udhibiti wa shughuli zote za utafutaji uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi nchini (PURA) waja na mpango mkakati wa kujenga mazingira bora yanayovutia kwa wawekezaji wa sekta ya mafuta na gesi wanaokuja kufanya utafiti na uwekezaji nchini. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Petroleum Upstream Regulatory Authority ( PURA ) Mhandisi Charles Sangweni ameyasema hayo leo Jijini Dar es salaam wakati akitembelea maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba 2024) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam. Amesema wanatarajia kutangaza maeneo watakayowashawishi na kuwavutia wawekezaji kuwekeza katika Sekta…

Read More

Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi Askari wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha ambao wamehitimu mafunzo ya udereva leo Julai 12, 2024 wametakiwa kuzingatia mafunzo waliyopewa sambamba na kwenda kuwa mabalozi wazuri kwa kuhakikisha wanafuata sheria za usalama barabarani Mkuu wa Operesheni za Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Salvas Makweli ambaye alimwakilisha Kamanda wa Polisi Mkoani humo ameyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya udereva yaliyoratibiwa na Jeshi la Polisi na kufanyika katika Chuo cha Ufundi Arusha. ACP Makweli amebainisha kuwa Askari hao ambao wamefuzu mafunzo ya udereva wataenda kuwa msaada mkubwa hasa ikizingatia…

Read More

Na Geofrey Stephen .Arusha Mkuu wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro Christopher Timbuka amesema itafikapo Agust mwaka huu wataenda kwenye vyanzo vya maji vya Somili na Urundini kuangalia upatikanaji wa maji namna gani ya ugawaji maji kati ya makundi mawili ya muekezaji pamoja na Wananchi. Haya yamesemwa katika mkutano wa hadhara wa Wananchi Kijiji cha Namwai Wilayani humo ambapo Mkuu huyo alifika kusiliza malalamiko kwamba muekezaji wa kampuni moja ya kuku amepewa maji mengi na hofu yao kwamba maji kwenye mfereji wao wa umwagiliaji yatapungua na kusabishia mazao yao kukauka. Mkuu huyo Akizungumza katika mkutano huo iliofanyika katika ofisi ya…

Read More