Author: Geofrey Stephen

KIAPO ! Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Fatma Abubakar Mwasa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2022.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Halima Omari Dendego kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2022. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Albert John Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti,…

Read More

Na Geofrey Stephen Karatu . Waziri wa Maji,Jumaa Aweso ametatua mgogoro uliodumu kwa muda mrefu wilayani Karatu baada ya kuamuru kuwepo kwa chombo kimoja kitakachosimamia utoaji wa huduma ya maji katika Mji huo huku akiagiza bei ya maji inayostahili kutozwa kwa sasa ni sh1,300 kwa uniti1 badala ya sh,2,000 hadi sh 3,000. Aweso ameagiza kuungana kwa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Karatu (KARUWASA) na Mamlaka ya Utoaji wa Huduma ya Maji Vijijini (KAVIWASU) na kutengeneza chombo kimoja ambacho kitatoa huduma kwa wananchi kwa maslahi ya wananchi wa Karatu. Hatahivyo waziri Aweso alitamka kwamba Rais Samia Hassan Suluhu…

Read More

Mwandishi wa A24Tv Arusha . Katika hali isiyo ya kawaida vurugu zimeibuka katika msiba wa watoto wawili wa matajiri jijini Arusha ambao walikuwa ni wachumba waliofariki ajalini baada ya mwandishi wa habari kutoka AyoTV kunyang’anywa camera. Mbali na kunyang’anywa camera mwandishi huyo alinyang’anywa kadi na kisha kuvunjwa na ndugu wa karibu akiwemo mdogo wa marehemu,Brighton Temu maarufu kama “Bonge “. Vurugu hizo zimefuatia mara baada ya mwandishi huyo,Gedfrey Thomas kutinga msiba ni kwa marehemu, eneo la KwaMrefu majira ya saa 10:30 leo jioni kufuatilia tukio la kifo cha mtoto wa Tajiri Denso. Taarifa zimeeleza kwamba mara baada ya mwandishi huyo…

Read More

Na Mwandishi wa A24Tv Arusha . Askofu wa kanisa la Anglican Dayosisi ya Mt,Kilimanjaro,Stanley Hotay amesema ya kwamba Afrika ikiwemo Tanzania ina rasilimali za kutosha na kusema ni wakati wa kuwafundisha wananchi kujenga desturi ya kujitegemea. Askofu Hotay alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa maadhimisho ya miaka 25 ya shirika la Here’s Life Africa Mission zilizofanyika katika kanisa hilo jijini Arusha. Sherehe hizo ziliwajumuisha washirika wa makanisa ya kiinjili hapa nchini ,nchi za Afrika Mashariki ,kati pamoja na Afrika Magharibi. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya sherehe hizo Askofu Hotay ambaye pia ni mkurugenzi wa shirika hilo…

Read More

Na .Mwandishi wanA24Tv Arusha Umoja wa nchi zinazozalisha almasi barani Afrika (ADPA) zimekubaliana kupitia upya na kurekebisha katiba na miongozo ya umoja huo kwa kuwa ile ya awali inepitwa na wakati. Hayo yamesemwa leo na waziri wa madini nchini,Dotto Biteko katika mkutano wa ADPA unaondelea jijini Arusha. Akizungumza na waandishi wa habari Waziri Biteko alisema kwamba tayari timu ya wataalamu imeshakamilisha nyaraka ambapo wataziwasilisha kwenye baraza la mawaziri ili ziweze kupitiwa . Waziri Biteko alisema kwamba wamejiridhisha kwamba nyaraka hizo zinahitaji marekebisho ili ziweze kuendana na wakati. “Leo zege halilali tunataka kuhakikisha tunakamilisha nyaraka za kuongoza ADPA ili kupitisha…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha SERIKALI imeeleza kwamba katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ugonjwa ya Saratani umeongezeka na kuwa tishio hapa nchini ambapo takwimu za mwaka jana 2021 zikionesha wagonjwa wapatao 14,136 waligundulika kuwa na Saratani ukilinganisha na mwaka 2020  wagonjwa walikuwa 12,000 tu. Akizungumza katika kongamano la sayansi la Saratani, jijini hapa,Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Saratani Ocean Road dkt Julius Mwaiselage ,ambaye alimwakilisha waziri wa afya ,Ummy Mwalimu,aliwataka wataalamu kutumia jitihada mbalimbali katika kudhibiti ugonjwa huo ambao unatishia mustakabali wa maisha kwa watanzania. Alisema magonjwa ya Saratani yanachangiwa zaidi na aina mbalimbali za maisha ikiwemo,ulaji usiofaa, kutofanya mazoezi ,unene…

Read More

Na Moses Mashalla, Baraza la madiwani la halmashauri ya jiji la Arusha limempitisha naibu meya wa jiji la Arusha,Veronica Hosea kwa kura 32 na kumfanya kutetea kiti chake kwa mara ya pili mfululizo. Mbali na kumchagua kiongozi huyo pia baraza hilo limewachagua wenyeviti wa kamati mbalimbali za halmashauri hiyo ambapo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)hakikuweka mgombea. Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo msimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni mstahiki meya wa jiji la Arusha,Maximillian Iranqe alisema madiwani walimpitisha Hosea kuwa naibu meya ambapo alijipatia kura 32 za ndiyo na hakuna kura iliyoharibika. Hatahivyo,meya huyo alisema kwamba mara baada ya uchaguzi…

Read More