Author: Geofrey Stephen

Na Geofrey Stephen Arusha . Waziri wa madini nchini,Dotto Biteko amesema kwamba licha ya changamoto ya janga la UVIKO-19 Tanzania imeendelea kufanya vizuri katika mauzo ya madini aina ya almasi katika soko la dunia. Waziri Biteko ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano wa tatu wa dharula wa baraza la mawaziri wa jumuiya ya nchi za Afrika zinazozalisha almasi(ADPA) unaofanyika jijini Arusha. Akizungumza katika mkutano huo waziri Biteko alisema kwamba baada ya janga la UVIKO-19 bei ya almasi duniani ilianguka na kupanda dhahabu lakini kwa sasa almasi imepanda juu na kuifanya Tanzania kuendelea kufanya vizuri duniani. Waziri Biteko amesema kuwa…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha. Viongozi wa dini pamoja na wazee wa kimila (Malaigwanan) wamesema wako  mstari wa mbele kuhamasisha jamii kushiriki katika zoezi la kuhesabiwa huku akiwataka kutoweka imani tofauti katika zoezi la Sensa litakalo anza mapema mwezi Agosti mwaka huu  Hayo yameelezwa julai 27 jijini Arusha na Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Arusha,Abel Mtupwa wakati akizungumza katika semina ya viongozi wa dini na mila mkoa wa Arusha iliyoandaliwa na Taasisi TWARIQATUL QADIRIYA JAILANIYA ARRAZAQIYA Tanzania . Mtupwa amesema kuwa,ni wajibu wa kila kiongozi kushirikiana kwa pamoja kila mmoja kwa nafasi yake ili watu waweze kushiriki kwa wingi katika zoezi…

Read More

Moses Mashalla, Sakata la gari lililoshikiliwa kwa tuhuma za kubeba madawa ya kulevya limeibuka tena ndani ya kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya Jiji la Arusha kilichofanyika leo katika ukumbi wa jiji. Gari hilo lenye nambari STJ 7333 lilishikiliwa mwanzoni mwa mwezi Juni mwaka huu na jeshi la polisi wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro likiwa na shehena ya mirungi ambapo linashikiliwa mpaka sasa. Akiibua hoja hiyo ndani ya kikao hicho diwani wa kata ya Ngarenaro,Isaya Doita aliuliza nini hatma ya gari hilo ambalo lilikamatwa likiwa na shehena ya mirungi. “Mheshimiwa Mwenyekiti gari hili mpaka sasa linashikiliwa na hatujui linarejeshwa…

Read More

YANGA na Sportpesa zasaini Mkataba mpya wa Udhamini KLABU ya Yanga SC, imesaini mkataba mpya wa Udhamini Mkuu na Kampuni ya kubashiri ya Sportpesa Tanzania, wenye thamani ya Tsh 12.3B kwa miaka mitatu (3), ambayo ni sawa na 4.1B kwa kila mwaka. Hili ni ongezeko la Tsh bilioni 2 kwa mwaka kutoka kwenye mkataba awali wa bilioni moja kwa mwaka mmoja. Sambamba na Fedha hizo ambazo Yanga itavuna, pia Bonus zitatolewa kama ilivyoainishwa kwenye mkataba ambapo Yanga ikifanikiwa kuwa Bingwa wa Ligi Kuu atapata Bonus ya 150M. Yanga ikifanikiwa Nusu Fainali Azam Sports Federation Cup (ASFC) itapata Bonus ya 75M na…

Read More

  Na Mwandishi wa A24Tv .NCAA Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Prof. Eliamani Sedoyeka tarehe 26 Julai, 2022 amefanya ziara katika ofisi za NCAA Karatu Mkoani Arusha kwa lengo la kukutana na Menejimenti kujadiliana masuala mbalimbali ya kuboresha utendaji kazi. Prof. Sedoyeka ameeleza kuwa kufuatia ongezeko la wageni ni muhimu kuhakikisha kuwa mda wote mitambo inakuwepo barabarani kwa ajili ya kurekebisha sehemu korofi ili kuboresha mawasiliano ya barabara kwa wageni mda wote. “Kwa sasa Ngorongoro ni moja ya maeneo yanayotembelewa na wageni wengi, Utaratibu mliouanza wa kuweka mitambo ya kurekebisha sehemu korofi uendelee ili kuhakikisha barabara katika…

Read More

Ujumbe wa wataalamu kutoka Wizara ya Elimumsingi ya Afrika Kusini umetembelea shule ya Msingi Chief Albert Luthuli iliyopo Mazimbu Mkoani Morogoro. Shule hii iko katika moja ya eneo waliloishi wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini wakati wa harakati za ukombozi wa nchi hiyo. Akiwa Shuleni hapo Mkuu wa Msafara huo, Enoch Rabotapi ambaye ni Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Elimu ya Ualimu nchini humo (Chief Director Teacher Development) ameahidi ushirikiano kati ya shule hiyo na baadhi ya shule zitakazobainishwa nchini Afrika Kusini kwa kubadilishana uzoefu na walimu. “Uhusiano wa nchi ya Tanzania na Afrika ya Kusini ni wa muda mrefu, na…

Read More

Moses Mashalla, Watendaji mbalimbali wa wizara ya habari,mawasiliano na teknolojia ya habari wanakutana jijini Arusha kuweka mipango ya kutekeleza bajeti ya wizara hiyo sanjari na kutathimini changamoto mbalimbali. Hivi karibuni bunge la jamhuri lilipitisha bajeti ya wizara ya habari,mawasiliano na teknolojia ya habari jumla ya kiasi cha sh,282.05 kama matumizi ya kawaida na miradi mbalimbali ya maendeleo. Akizungumza katika kikao hicho naibu waziri wa habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Mhandisi Mathew Kundo alisema kwamba wamekutana kwa lengo la kufanya tathmini na mpango wa kutekeleza bajeti hiyo ambayo ilipitishwa Hivi karibuni na bunge la jamhuri. Naibu waziri huyo alisema kwamba…

Read More