Author: Geofrey Stephen

Happy Lazaro,Arusha . Wanawake wanaochipukia kwenye nafasi mbalimbali za uongozi wametakiwa kuwa na udhubutu wa kugombea nafasi mbalimbali na kuwa mstari wa mbele katika kutoa maono kwani wana mchango mk.ubwa katika jamii . Hayo yamesemwa mkoani Arusha na Mbunge wa bunge la Afrika Mshariki ,Fatuma Ndangiza wakati akizungumza katika mdahalo wa kwanza wa Afrika Mashariki kuhusu wanawake kwa maswala ya uongozi bora . Aidha mdahalo huo uliwashirikisha wanawake wanaochipukia kwenye nafasi mbalimbali za uongozi na kufanyika katika makao makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki. Fatuma amesema kuwa,lengo la mdahalo huo ni kuwakutanisha vijana hao wanaochipukia kwenye uongozi kuweza kubadilishana uzoefu…

Read More

Na Richard Mrusha Kampuni ya mawasiliano ya Tigokwa nchini Tanzania, inatalajia kufanya uzinduzi wa simu mahiri za bei nafuu zaidi, ZTE A34 kwa ushirikiano na ZTE Tanzania kupitia Sako kwa Bako na Simu janja kwa Mpango campaign. Uzinduzi huu unaashiria hatua kubwa ya kusonga mbele katika dhamira inayoendelea ya Tigo ya kuunganisha watu ambao hawajaunganishwa na kuwapa wateja fursa ya kufurahia mtandao ulioboreshwa na mpana zaidi wa 4G nchini. Imelda Edward, Meneja wa Kifaa wa Tigo, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano huu wa kimkakati na ZTE Tanzania. “Ushirikiano wetu na ZTE ni uthibitisho wa dhamira yetu ya kupunguza mgawanyiko wa kidijitali…

Read More

Na Richard Mrusha Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Zuhura Yunus ametembelea Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Taasisi zake katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea kwenye Uwanja wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere, jijini Dar Es Salaam leo tarehe 5 Julai, 2024. Aidha, amehimiza watumishi Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kutatua changamoto za wananchi wanaotembelea banda hilo kwa ajili ya kupata huduma na uelewa masuala yanayotekelezwa na ofisi hiyo. Katika Maonesho hayo Naibu Katibu Mkuu ametembelea Idara, Vitengo na Taasisi zilizopo chini ya ofisi hiyo…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha . Mwenyekiti wa bodi ya Hoteli ya kitalii ya Parrot ya Jijini Arusha,  Abdallah Msele,amesema mradi huo wa hoteli hiyo umekamilika kwa 98% unatoa ajira rasmi 200 na zisizo rasmi 300 Ameyasema hayo leo kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa awali wa hoteli hiyo iliyopo barabara kuu ya col milditon kata ya kaloleni, kuwa uwekezaji wa Mradi huo ni kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan  katika swala Zima la Utalii Amesema Mradi huo ulianza mwaka 2004 ulikumbwa na changamoto na ulusimama hivyo mmiliki wake wa awali marehemu,Abdallah Idd Mshana,aliomba mikopo benki ya Uwekezaji na…

Read More

Na Richard Mrusha MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema inakwenda kuwekeza nguvu kubwa kwenye kuelimisha wafanyabiashara (walipa kodi)  hasa kuijua sheria ya kodi ya 2024/2025 Akizungumza na waandishi wa habari kwenye maoneaho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) jijini Dar es Salaam,Kaimu  Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano wa TRA Hudson Kamoga, amesema hatua hiyo itamwezesha mlipa kodi kulipa kodi bila shuruti. Amesema pia TRA itahakikisha inatumia mifumo zaidi katika shughuli zake ili kurahisisha huduma kwa wateja kwa wake. Amesema ni wakati wakuwahimiza  wafanyabiashara kutunza kumbukumbu kwa kutoa risiti za mashine…

Read More

Na Richard Mrusha MWALIMU wa Chuo cha VETA Kigoma Innocent Maziku ameiomba Serikali kupitia watafiti wake kutoka Wizara ya Afya kukifanyia utafiti kifaa cha kuboresha usikivu kwa watu wenye usikivu hafifu ili azalishe vifaa hivyo kwa wingi zaidi ili vigawiwe shuleni kwa watoto wenye changamoto hiyo. Akizungumza kwenye banda la VETA jijini Dar es Salaam kwenye .aoneaho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara Maziku amesema kifaa hicho alichoanza kukibuni oktoba mwaka jana,kimekamilika tangu Machi mwaka huu lakini anashindwa kuendelea kuvizalisha kwa wingi kwani bado hakifanyiwa utafiti wa kujua kama kina madhara ya kiafya kwa mtumiaji. Amesema kuna Idadi kibwa ya…

Read More

NA. Richard Mrusha Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu imejipanga kuhakikisha inaendelea kuwafikia wananchi wanaopata huduma katika banda jumuishi la ofisi hiyo wakati wa maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba kwa kuhakikisha wanapewa elimu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu ofisi hiyo pamoja na taasisi zilizochini yake. Ameyasema hayo tarehe 04 Julai, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ikiwemo la Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Wizara ya Fedha na taasisi zake,…

Read More

Na Richard Mrusha MKUU wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajab Mabele kutokana na mazingira ya uwekezaji kuboreshwa ,kumeifanya Tanzania kuwa mahali  salama pa kufanya biashara na uwekezaji. Akizungumza leo Julai 3 ,2024 na waandishi wa habari katika banda la JKT kwenye maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara ,Meja Jenerali Mabele amesema   hali hiyo imefanya watu wengi zaidi kuja kuwekeza hapa nchini. “Naipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira  mazuri ya kufanya biashara na hivyo watu wengi zaidi kuja kuwekeza hapa nchini na hivyo kuifanya Tanzania kuwa…

Read More

Richard Mrusha Dar es Salaam Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imesema itaendelea kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata huduma bora na kwa wakati unaotakiwa kwa lengo la kuwaletea maendeleo na Taifa kwa ujumla. Kauli hiyo imetolewa tarehe 03 Julai, 2024 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama wakati alipotembelea banda jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zilizopo chini yake katika maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (SABASABA) ili kujionea jinsi watumishi wa ofisi hiyo wanavyotoa huduma kwa wananchi na wadau kwa ujumla. Akiwa katika banda la…

Read More