Author: Geofrey Stephen

Na Mwandishi wa A24tv . Chama cha mapinduzi (CCM), Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro kimeitaka ugwaji wa Aridhi katika Kijiji cha Sanya station kata ya KIA Wilayani hapo kuzingatiwe sheria na taratibu ili kuepusha malalamiko kutoka kwa Wananchi Wananchi hao ni wale pamoja na vijiji vya Sanya station,Tindigani na chemka walioridhia kupisha eneo na kupewa fidia na Serikali baada ya kubainika kuwa kwenye eneo la Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA). Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya Wangub Maganda akiongea kwenye mkutano wa kuwasilisha na utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2020,2023 kata ya KIA iliyofanyika katika Kijiji…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv . Siha,Jeshi la Polisi Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro,linafanya operesheni ilikukamata wezi wanavunja na kuiba mali mbali mbali za Wananchi zikiwamo pikipiki,tv Radio jambo ambalo linarusisha juhudi za maendeleao nyuma Kutokana na zoezi hilo kuendelea Wananchi Wilayani humo wameipongeza Jeshi hilo kwani wameweza kufakiwa kupata baadhi ya mali zilizoibiwa pamoja na wannunuzi wa mali hizo za wezi. Mkuu wa Jeshi hilo Wilayani humo Zakia Shuma,kizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake,amesema zoezi hilo ni endelevu hadi uhalifu upungue na kuomba ushirikiano kwa Wananchi “Ni kweli tumeanza zoezi la kuwasaka wahalifu wakiwemo wezi wa mali za watu…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha . Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA),Mkoa wa Arusha,imewataka  wanafunzi wanaosoma kozi ya uhandisi  umeme, kuona umuhimu wa kuchukua leseni  inayotolewa na mamlaka hiyo ili kujiwekea mazingira mazuri na kulinda taaluma yao. Akiongea na  waandishi wa habari wakati wa utoaji wa semina  kwa wanafunzi wa kozi ya uhandisi umeme inayotolewa na EWURA katika chuo cha Ufundi Arusha(ATC). Lorivii Long’idu,Meneja EWURA kanda ya kaskazini akizungumza na vyombo vya habari juu ya elinu walio toa kwa wanafunzi wa chuo cha Atc Arusha  Meneja wa EWURA kanda ya kaskazini, Mhandisi Lorivii Long’idu alisema lengo la…

Read More

ELIMU YA POLISI JAMII KWA WATOTO Mkaguzi wa kata ya Ngarenaro jijini Arusha Mkaguzi Msaidizi wa polisi Tadey Tarimo leo tarehe 21/06/2024 amepita maeneo ya Mtaa wa Darajani na kutoa elimu kwa watoto wanaoishi katika mtaa huo Tarimo amewaasa watoto kucheza michezo salama hususani katika kipindi hiki cha likizo. Sambamba na hilo amewataka kutokukalia kimya vitendo vya ukatili na badala yake watoe taarifa haraka katika kituo cha Polisi cha Ngarenaro kwani kipo karibu na makazi yao. Aidha, amewataka kutowaogopa Polisi pindi wawaonapo kwani wapo kwa ajili ya kuwalinda. View 1 comment 6 hours ago . See translation

Read More

Na Mwandishi wa A24tv. Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt Hashil Abdallah amesema utekelezaji wa Mkataba wa Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA) katika kuondoa vikwazo visivyokuwa vya kiushuru na kufungamanisha Sera za Biashara kutachangia kuongeza mauzo ya nje, kuboresha uwiano wa biashara, kupatikana kwa soko la bidhaa za Tanzania nje ya Nchi na kukuza biashara na uchumi kwa ujumla. Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt Hashil Abdallah akiongea na Waandishi wa Habari baada ya ufunguzi wa Mkutano wa 17 Makatibu Wakuu wa AfCFTA unaofanyika kuanzia Juni 18 – 22, 2024 ukifuatiwa na Mkutano ngazi ya…

Read More

Na Richard Mrusha Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amefungua rasmi Maonesho ya kwanza ya asali kufanyika nchini Tanzania (Honey Show) huku akihamasisha Watanzania kujitokeza kuchangamkia fursa za ufugaji nyuki na uzalishaji wa asali ili kukuza vipato vyao. Ameyasema hayo leo Juni 19,2024 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Amesema lengo la Maonesho hayo yenye kaulimbiu “Beyond Hives, Beyond Borders” ni kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa ufugaji nyuki, uongezaji thamani na uzalishaji wa asali. Amesema sekta hiyo ndogo ya ufugaji nyuki ina nafasi kubwa katika uchumi, ajira, utunzaji wa mazingira,…

Read More