Author: Geofrey Stephen

Na Doreen Aloyce , Dodoma SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo katika maandalizi ya kuunda timu ya wataalamu itakayoweza kutembelea taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100 kwa siku ikiwa ni kutekeleza agizo la Dkt.Rais Samia Suluhu Hassan la kusitisha matumizi ya kuni na mkaa ifikapo Januari 2024. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Seleman Jaffo jijini hapa wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua za utekelezaji wa katazo la matumizi ya kuni na mkaa ambapo amesema lengo la maelekezo ya Rais Samia ni Kupunguza madhara ya kiafya…

Read More

Na Geofrey Stephen , Arusha . JESHI la polisi kikosi cha usalama barabarani kwa kushirikiana na Chuo cha ufundi Arusha (ATC) wametoa mafunzo maalumu kwa wakuu wa usalama barabarani na wakaguzi wa magari na watahini wa madereva kutoka mikoa yote Tanzania na Zanzibar kuhusu matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa sheria za usalama barabarani. Akizungumza mkoani Arusha katika mafunzo hayo ya siku mbili ambayo yanaendelea mkoani hapa,Mkuu wa chuo cha ufundi Arusha ,Prof .Musa Chacha amesema kuwa lengo la mafunzo hayo kwa jeshi la polisi ni kuongeza ujuzi katika ukaguzi wa magari ili watanzania wanaposafiri waweze kuwa salama. Prof .Chacha…

Read More

Na Mwandishi A24tv. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia prof. Adolf Mkenda amesema Taifa linahitaji Walimu bora na mahiri katika kufundisha pamoja na uwezo wa kukaa na kuwalea vizuri watoto wa Kitanzania ili wafikie malengo yao na kusaidia nchi katika nyanja mbalimbali. Waziri Mkenda ametoa rai hiyo Februari 19, 2024 Mkoani Tanga wakati akifungua Mafunzo ya Kitaifa ya kuwajengea uwezo Walimu Wakuu wa Shule za Msingi wapatao 347, kutoka Wilaya ya Korogwe Mji, Korogwe Vijijini na Lushoto kuhusu Uongozi, Usimamizi wa Shule na Utawala Bora yanayofanyika katika Chuo cha Ualimu Korogwe. Prof. Mkenda ameeleza kuwa mageuzi ya Elimu ndio agenda…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv . Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali inaiangalia sekta binafsi kwa mtazamo chanya wa kuwa mdau muhimu wa uchumi na maendeleo. Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipofungua Mkutano mkuu wa kumi na tano(15) wa Jumuiya ya Kitaifa ya Wafanyabiashara Zanzibar katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, uwanja wa ndege Zanzibar tarehe: 19 Februari 2024. Aidha Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa tayari kazi ya kuandaa sheria inayohusisha maendeleo ya sekta binafsi inaendelea chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara ikisimamiwa na Sekretarieti ya Baraza la Taifa la Biashara. Vilevile Rais…

Read More

Karibu kutazama matukio katika picha viongozi wakiongozwa na Mh Rais Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya Hayati Edward Lowasa kijijini Ngarashi Wilayani Monduli Mkoani Arusha . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua kwenye kaburi la Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowassa katika mazishi yaliyofanyika nyumbani kwa Marehemu Monduli Mkoani Arusha tarehe 17 Februari, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka udongo kwenye kaburi la Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowassa Monduli Mkoani Arusha tarehe 17 Februari, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi amewahimiza malezi bora katika jamii ili kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo matumizi ya dawa za kulevya, wizi, ubadhirifu wa mali za umma, udhalilishaji na ulevi. Rais Dk.Mwinyi amesema malezi bora yanaanzia ngazi ya familia, pia amewataka wazazi na walezi Kuwalea vijana katika malezi mema yenye maadili. Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika ibada ya Sala ya Ijumaa Msikiti wa Makuti Kisiwandui Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe :16 Februari 2024. Rais Dk.Mwinyi ameshiriki katika ibada ya sala…

Read More