Author: Geofrey Stephen

Na Mwandishi wa A24tv . Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Serikali inawatarajia Wahitimu katika mafunzo ya elimu kuwa mabalozi wa utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 Toleo la 2023. Prof. Mkenda ametoa rai hiyo Disemba Mosi, 2023, Bagamoyo Mkoa wa Pwani wakati akizungumza kwenye mahafali ya 31 ya Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM). “Katika kipindi hiki, tunawategemea sana kwenda kutusaidia kutekeleza mageuzi ambayo yameanishwa katika Sera mpya ya Elimu, pamoja na jukumu la kufundisha mtaenda kusimamia mabadiliko ya elimu nchini” Alisema Prof. Mkenda. Amesema Serikali imeanza mchakato wa…

Read More

Na mwandishi wetu Arusha. Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), imewataka wafanyabiashara kuhakikisha kuwa wanasajili logo zao kabla ya kuanza kuzitumia  ili kuepuka usumbufu wa kuibiwa logo na wafanyabiashara wengine na kisha kujikuta katika mgogoro wa kibiashara. Afisa Usajili wa BRELA  Bi. Julieth Kiwelu ameeleza hayo Desemba,1, 2023, Maafisa hao walipowatembelea baadhi ya wafanyabiashara wa jijini Arusha ili kujua changamoto wanazozipata wakati wa kupata huduma mbalimbali za Taasisi kwa lengo la kuzipatia ufumbuzi. Wakiwa katika Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo  (SIDO),  Bi. Kiwelu amesema pamoja na kwamba huduma zote za BRELA zinatolewa kwa njia ya mtandao, bado kuna…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv . Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhandisi Zenna Ahmed Said, ametoa wito kwa wanawake wote wanaojihusisha na biashara kushiriki Kongamano la Pili la Wanawake katika Biashara chini ya Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA) linalotarajiwa kufanyika tarehe 06 hadi 08 Disemba, 2023 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu Kiongozi huyo amayasema hayo Novemba 30,2023 akiwa katika kikao cha maandalizi ya Kongamano hilo ambalo Tanzania ni mwenyeji na linaandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Sekretarieti ya…

Read More

Doreen Aloyce, Dodoma Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara (Mb) Exaud Kigahe amesema Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri zote nchini ipo tayari kuwasaidia wafanyabiashara na wajasiliamali katika nyanja mbalimbali ili waweze kutimiza ndoto zao za kiuwekezaji na kibiashara. Mheshimiwa Kigahe ameyasema hayo ,Disemba Mosi Mwaka 2023 Jijini Dodoma wakati akifungua Kongamano la Biashara na Uwekezaji la Jiongeze lililoandaliwa na Wasafi Media. Aidha amesema katika kutatua changamoto hiyo Serikali imeanzisha kitengo kamili kinachoshughulikia maswala ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara katika kila Halmashauri kote nchini. Sanjari na hilo,amebainisha,kuwa Serikali imeanzisha Dirisha la Kielektroniki la Kuwahudumia Wawekezaji mahala pamoja (Tanzania Electronic Investment Window)…

Read More

Na Mwandishi wa A24Tv . WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amebainisha kuwa, elimu inayotolewa kupitia masomo ya dini ni tofauti na ile ya masomo mengine kwani elimu hiyo inahusisha masuala ya imani na hugusa zaidi hisia. Prof. Mkenda alisema hayo Novemba 30, 2023 katika uzinduzi wa Tanzania Islamic Studies Teaching Association (TISTA) pamoja na makabidhiano ya muhtasari na kitabu cha kwanza cha mwanafunzi cha Elimu ya dini ya Kiislamu, tukio lililofanyika katika ukumbi wa Mfalme Mohamed BAKWATA makao makuu Kinondoni Dar es Salaam. “Mitaala ya dini ni ya kipekee, ni tofauti na mitaala ya somo la…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv Viongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu wamekagua maandalizi ya kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani Desemba 1, 2023 katika Viwanja vya Morogoro Sekondari ambapo maandalizi hayo yamekamili.Katika ukaguzi huo waliongozwa na Mhe. Jenista Mgahama ambaye ndiye Waziri mwenye dhamana ya uratibu. Ikumbukwe maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani hufanyika kila mwaka ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema “Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI”. Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa. Mwisho .

Read More

Na Mwandishi wetu Viongozi wa dini nchini wamehimizwa kuwaelimisha na kuwajenga vijana katika maadili mema, kuwaepusha na maambukizi ya VVU na kudhihirisha jitihada za pamoja kati ya Taasisi za dini na Serikali katika kulinda na kuhamasisha vijana kutambua hali zao za maambukizi ya VVU na kupata elimu ya Afya ya Uzazi. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi katika ufunguzi wa Mdahalo kati ya Vijana na Viongozi wa dini uliofanyika Tarehe 29, 2023 mkoani Morogoro ikiwa ni sehemu ya shughuli mbalimbali zinazoendelea kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI…

Read More

HABARI PICHA Na mwandishi wetu Dkt. Yonazi aridhishwa na maandalizi ya Kuelekea Siku ya UKIMWI Duniani Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi ametembelea mabanda mbalimbali na kujionea maandalizi yaliofanywa na wadau mbalimbali kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yatakayofanyika 1 Disemba,2023 katika Viwanja vya Morogoro Sekondari ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa(mb) Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI” Aidha ametumia nafasi hiyo kuwahimiza wananchi kujitokeza katika maadhimisho hayo na kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali…

Read More