Author: Geofrey Stephen

Na Geofrey Stephen Arusha . Tamasha kubwa la kihistoria la wanawake festival kutikisa viunga vya jiji la Arusha na Mkoa kwa ujumla ambapo Waziri wa Mali asili na utalii Anjela Kairuki anatarajiwa kufungua tamasha la hilo la aina yake la  Wanawake festival litakalofanyika November 17 jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa Simba hall  Aicc. Tamasha linalenga kuwezesha kufikia idadi ya watalii milioni Tano ifikapo mwaka 2025 Akizungumza na vyombo vya habari jijini Arusha mwenyekiti wa tamasha hilo Nengasu Werema amesema kuwa wameamua kuunga serikali mkono katika jitiada za kutangaza utalii. Alisema kuwa wao kama wanawake watafanya tamasha hilo ambalo…

Read More

Na Richard Mrusha Mahenge SERIKALI imeombwa kupeleka huduma ya mawasiliano ya simu za kiganjani katika kijiji cha Epanko Halmashauri ya Mji Mahenge wilaya ya ulanga Mkoani Morogoro ili kurahisha mawasiliano katika uendeshaji shughuli za uchimbaji madini ya vito (Spinel) katika kijiji hicho. Mbali na hilo pia imeombwa kuboresha huduma ya upatikanaji wa nishati ya umeme wa uhakika katika maeneo ya migodi hili kuweza kusaidia kutozalisha kwa hasara kama ilivyo sasa. Akizungumza wa waandishi wa habari wakati walipotembelea mgodi wa Franone Mining and Gems wanaozalisha madini ya Spinel kwa lengo lakupata elimu kuhusu madini hayo Meneja Mgodi Elias Thomas amesema kuwa…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv. #Prof. Nombo aridhishwa na maendeleo ya ujenzi, amtaka Mkandarasi kuongeza nguvukazi ili kukamilisha jengo kwa wakati. Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameielekeza Kampuni ya China ya CRJE inayotekeleza mradi wa ujenzi wa majengo ya Wizara ya Elimu ya Sayansi na Teknolojia kuongeza nguvu kazi na muda wa kazi ili kuhakikisha jengo hilo linakabidhiwa ifikapo Disemba 15, 2023 kulingana na makubaliano ya mkataba. Prof. Nombo ametoa maelekezo hayo Novemba Mosi, 2023 wakati alipotembelea na kukagua ujenzi wa jengo jipya la Ofisi za Wizara hiyo lililopo katika Mji wa kiserikali Mtumba ili…

Read More

Kesi dhidi ya sabaya kukatiwa rufaa na jamhuri  imenguruma leo katika mahakama kuu kanda ya Arusha huku upande wa serikali wakieleza hoja zao saba  mbele ya  majaji watatu wa rufani Kesi  imesikilizwa kwa muda wa masaa saba ambapo pia mabishano ya kisheria kwa upande wa utetezi wa sabaya na serikali ulikua mkubwa ambapo majira ya saa kumi na moja kesi hiyo ilimalizika na huku majaji wakisema maamuzi ya rufani hiyo itatolewa baadae kupitia kwa msajili wa mahakama kutoa taharifa kwa mawakili wa pande zote mbili Kesi ilikua ikisikilizwa na majaji watatu wakiongozwa na Mwenyekiti Jaji Jacobs Mwambegele, Jaji Ignas Kitusi…

Read More

Shirika la Uraia na Msaada wa Kisheria CILAO linakusudia kukata rufaa kupinga maamuzi ya mahakama yaliyoipa ushindi  Jamhuri dhidi ya mlalamikaji Odero Charles Odero aliyekuwa akipinga mtuhumiwa kukamatwa na kufungulia mashtaka bila upelelezi kukamilika ,akidai  imejaa ukiukwaji wa haki za kibinadamu. Aidha shirika hilo tayari limewasilisha maombi hayo ya kufungua shauri hilo nje ya muda yanayotarajiwa kusikilizwa  Novemba 2 mwaka huu katika mahakama Kuu ya Tanzania masijala ndogo ya Dar es salaam. Akiongea na waandishi wa habari mlalamikaji ,Odero Charles Odero ambaye pia ni mkurugenzi wa shirika la CILAO . alisema mwaka 2021 alifungua  kesi ya kikatiba mahakama kuu ya…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv . Moshi.Baraza la Madiwani Manispaa ya Moshi limepata taharuki baada ya aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Moshi na Diwani wa Kata ya Bomambuzi Mh Juma Raibu kuingia na fimbo iliyodhaniwa ni ile ilikuwa ikitumika na Mwalimu Nyerere jambo ambalo liliamisha mjadala uliokuwa unajadiliwa na kuijadili fimbo hiyo huku imani za kishirikina zikitajwa huku wengine wakishindwa kutoa taarifa kwa usahihi na kuaingizia fimbo hiyo Akizungumza nje ya kikao cha baraza Katibu wa Baraza la madiwani Witness Mzirai alisema fimbo hiyo iliibua taharuki huku akisema kuwa fimbo hiyo haina shida yoyote kama baadhi ya watu walivyoihusisha na imani…

Read More

Na Geofrey Stephen Arusha  Wamshukuru Rais Samia baaaba kufanyiwa  upasuaji wa Nyonga na Magoti bure katika hospitali  ya Arusha Lutheran Medical Center ALMC jiji Arusha,kupitia mpango wa mama Samia Love uliotekelezwa  na madaktari bingwa kutoka nchini Marekani ,wamemshukuru Rais Samia  kutokana na maendeleo yao mazuri na kumwomba huduma hiyo iwe endelevu ili kuwasaidia watanzania wengine wenye changamoto kama hiyo. Akiongea na waandishi wa habari baada ya kutembelewa nyumbani kwake na taasisi ya Samia Love inayoratibu huduma hiyo hapa nchini,mmoja ya magonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa Goti,Ester Mengowo mkazi wa Mbulu Mkoani Manyara Alisema kuwa ujio wa madaktari hao imekuwa faraja kubwa…

Read More