Author: Geofrey Stephen

Na Mwandishi wa A24Tv . Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Ngorongoro Mkoani Arusha imemhukumu kifungo cha maisha jela mfugaji, Ole Sure Miliari(19) mkazi wa wilaya hiyo,baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumlawiti Mwanafunzi wenye umri wa miaka 8 na kumsababishia kutokwa damu nyingi sehemu zake za siri. Kesi hiyo namba 16 ya mwaka ,2023 Miliari alitenda kosa hilo katika wilaya hiyo kwa kumlawiti mwanafunzi huyo ambapo mara baada ya uchunguzi wa Daktari iligundulika aliharibiwa vibaya katika maumbile yake nakupelekea kufungwa nepi (Pampas) kutokana na kitendo hicho cha kinyama . Akisoma hukumu hiyo jana Oktoba 5,2023 Hakimu Mkazi wa…

Read More

Na mwandishi wetu Idara ya Menejimenti ya Maafa Nchini yashirikisha ujuzi wa masuala ya usimamizi wa maafa kwa wanafunzi na wakufunzi kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Jeshi la Ulinzi la Malawi walifanya ziara yao ya mafunzo nchini Tanzania Akizungumza wakati wa kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es salaam kilicholenga kubadilishana uzoefu katika usimamizi wa maafa kati ya wataalam wa Ofisi ya Waziri Mkuu na ujumbe wa wanafunzi na wakufunzi kutoka chuo hicho, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Luteni Kanali Selestine Masalamado amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea…

Read More

Na Mwandishi wa A24Tv. Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo leo Oktoba 5, 2023 amekabidhiwa Uenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Afrika (AICAD) inayohusika kujengea uwezo Vyuo Vikuu na Jamii katika masuala mbalimbali ikiwemo Kilimo, maji na kuongeza thamani. Prof. Nombo anapokea nafasi hiyo kutoka Kenya kwa ajili ya kuongoza kwa miaka miwili kuanzia mwaka 2023. Akizungumza baada ya kukabidhiwa Prof. Nombo ameshukuru na kupongeza Uongozi uliopita kwa kazi nzuri, huku akisisitiza nia yake ya kusimamia malengo ya Taasisi hiyo kikamilifu. ‘’Namshukuru Mwenyekiti aliyemaliza muda wake kutoka Kenya, hakika umeiongoza Taasisi hii vizuri, mmetusaidia kufika…

Read More

Bertha Mollel, Tanga Wakati Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA) ikitangaza ongezeko la mvua za vuli kuzidi kiwango ikiambata na upepo mkali ‘El-nino’, serikali Wilayani Same imeanza kuchukua tahadhari juu ya madhara yake. Tahadhari ya mvua hizo zilizotolewa na TMA, zinaonyesha kuwa mvua hizi zitakazoanza mwezi Octoba hadi desemba, zitakuwa za juu ya wastani na zitaambatana na upepo mkali na magonjwa ya mlipuko. “Mvua hizi kawaida mbali na magonjwa lakini pia yataleta mafuriko hivyo sisi kama Wilaya ya Same tumeanza kujiandaa na madhara yatakayoweza kujitokeza ikiwemo kusaka vifaa vya uokozi na uokoaji” alisema katibu tawala Wilaya ya Same Upendo…

Read More

Na Mwandishi wa A24Tv Jumla ya vijana 6,000 kutoka Shirika la Suma JKT la Jeshi la Wananchi Tanzania,(JWTZ) wameanza kuwasili wilayani Handeni mkoani Tanga kwaajili ya shughuli ya ujenzi wa nyumba 5,000 katika kijiji cha Msomera. Akizungumzia kuhusu ujio wa vijana hao, wilayani Handeni,Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa,(JKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele amesema shughuli yao itakuwa ni ujenzi wa nyumba hizo na tayari Vijana 500 wamesharipoti kwenye mradi na wengine wanaendelea kuingia. Amesema tayari wameshapokea fedha kutoka uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro,kwaajili ya kujenga nyumba hizo ambapo muda wa ujenzi utakuwa ni miezi sita kuanzia Oktoba 2023 hadi…

Read More

Na Mwandishi A24Tv . Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Dkt. Seleman Jafo amelipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC kwa usimamizi mzuri wa Sheria ya Mazingira katika mradi wa kufua umeme wa bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP). Pongezi hizo zimekuja mara baada ya Waziri huyo kuzuru eneo la mradi kwa lengo la kujiridhisha na hatua za ujenzi zilipofikia sambamba na suala la utunzaji na uhifadhi wa Mazingira katika eneo hilo ” Mradi huu ni mkubwa wenye shughuli kubwa na nyingi zinazozalisha taka za kila aina na idadi ya watu…

Read More

Na Mwandishi A24Tv Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Exhaud Kigahe (Mb.) ameziagiza BRELA, SIDO na Taasisi husika kufika katika Ngazi za Halmashauri ili kuwawezesha Wafanyabiashara. Amesema hayo Octoba 3,2023 akiwa anafunga Kongamano la Biashara na Uwekezaji wilayani Pangani Jijini Tanga lililofanikiwa kuwakutanisha wafanyabishara mbalimbali mkoani Tanga. Aidha, Kigahe amesema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na kuhakikisha sekta binafsi zinafanya vizuri katika maendeleo ya biashara na uchumi.³ Aidha amewataka wafanyabiashara, Wadau wa Maendeleo na Wajasiliamali kuchangamkia Fursa za utalii, kilimo, ufugaji na uchumi wa bluu katika wilaya ya Pangani Vilevile, Kigahe amesema…

Read More