Author: Geofrey Stephen

Na Richard Mrusha Geita AFISA mauzo na usambazaji kutoka Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko Kanda ya ziwa Francisco Amos Amesema kuwa walikuwa ni moja ya Taasisi ya Serikali ambayo walishiriki maonesho ya madini mkoani Geita nakwamba kwao yamekuwa yamafanikio makubwa. Amesema kuwa wananchi wengi walipata fursa ya kufika kwenye Banda lao na Kwa ujumla walipenda huduma na bidhaa ambazo walikuja nazo kwenye maonesho hayo. Amos ameyasema hayo septemba 30 mwaka huu katika hitimisho la maonesho ya sita ya kimataifa ya teknolojia ya madini ambayo yanafanyika Kila mwaka mkoani humo . Amos Amesema licha ya kwamba ni mara yao ya…

Read More

Mwandishi wetu. Michuano ya 16 ya Chemchem CUP 2023 ambayo inalenga kupiga vita ujangili wa Twiga imezinduliwa Jana katika eneo la hifadhi ya jamii ya Burunge WMA wilayani Babati mkoa Manyara. Akizungumza katika uzinduzi huo,Mkuu wa wilaya ya Babati.Lazaro Twange kwa niaba ya Mkuu wa mkoa,alisema michuano hiyo licha ya kuinua vipaji vya michezo lakini inaendeleza uhifadhi. Twange alisema vijiji 10 ambavyo vinaunda Burunge WMA,vinapaswa kushirikiana na Taasisi ya chem chem ambayo imeweza shughuli za utalii na uhifadhi katika eneo hilo. “Tunatarajia nyie muwe mabalozi wazuri wa uhifadhi ,mtowe taarifa za wanaojihusisha na ujangili lakini pia muendelee kunufaika na uhifadhi”alisema.…

Read More

Na. Anangisye Mwateba-Mafia Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Majaliwa ameagiza Wizara ya malisili na utalii kupitia Bodi ya utalii kutangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana katika kisiwa cha Mafia. Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo wakati akifunga Maonesho ya Utalii na Uchumi wa Bluu katika kisiwa cha Mafia. Akitoa takwimu za idadi ya watalii waliokitembelea Kisiwa hicho tangu mwaka 2020 Waziri Mkuu amesema watalii 14,153 na walifika kisiwani Mafia na kuingiza kiasi cha shilingi bilioni 2.7 na kuongeza kuwa mafanikio hayo ni juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan…

Read More

Na. Costantine James , Geita. Mamlaka ya Maji na Usafi na Mazingira mjini Geita imesema imeandaa mikakati Madhubuti kuhakikisha miradi inayoendelea kutekelezwa na ijayo inakamilika kwa wakati uliopangwa Ili kuhakikisha kuwa wanatatua Changamoto ya upatikanaji wa Maji safi na salama kwa wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Geita. Hayo yamebainishwa na Meneja wa GEUSA Mhandisi Frank Changawa wakati akielezea mipango na mikakati mbele ya Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini alipotembelea banda la GEUWASA kwenye maonyesho 6 ya Teknolojia ya madini yanayofanyika Mjini Geita amesema kwa Sasa Maji yanatoka kwa mgao lakini miradi mingi inatekelezwa ukiwemo ule wa miji 28…

Read More

Na. Costantine James , Geita Shirika la uwakala wa meli Tanzania (Tanzania shipping Agency Corporation TASAC) wamewakumbusha wadau wa sekta ya madini wajibu wa TASAC kifungu Cha namba 7(1) Cha Sheria ya uwakala wa Meli sura 415 inayowapa TASAC majukumu ya kipekee “Exclusive Mandate” ya utoaji wa huduma ya uwakala wa forodha ,inatekeleza majukumu ya ukomboaji wa shehena katika maeneo mbalimbali ya forodha kwa bidhaa silaha na vilipuzi ,makinikia na kemikali zinazotumika kwenye kampuni za uchimbaji madini.TASAC wameongea hayo Leo Ijumaa September 29,2023 katika Maonesho ya sita (6) ya teknolojia ya Madini yanayofanyika viwanja vya Bombambili EPAZ mkoani Geita. TASAC…

Read More

Na Ahmed Mahmoud Umoja wa Wanasayansi ya Udhibiti wa Wadudu waharibifu wa Mazao nchini(TEA) umeeleza utaendelea kufanya utafiti zenye kuleta matokeo sahihi ya kukabiliana na Wadudu waharibifu ambao wanaleta athari kwa Afya za binadamu wanyama na Mazingira. Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania TPHPA Prof.Joseph Ndunguru katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wanasayansi waudhibiti wa visumbufu vya Mazao unaofanyika Jijini Arusha. Amesema kwamba uwepo wa majadiliano ya tafiti utasaidia kuongeza tija na kuboresha uzalishaji wa mifugo Mazao na hivyo kuongeza soko na usalama wa chakula nchini. “Mkutano huu ni Jukwaa la…

Read More

Na Mwandishi wa A24A24Tv Katika Mwaka wa fedha 2023-2024 Halmashauri imeendelea kusimamia na kutekeleza miradi mbali mbali ya Maendeleo na shughuli za serikali kupitia Mapato ya ndani na Ruzuku ya serikali kwa fedha zilizotolewa mwaka 2022-2023 na fedha za Mapato ya ndani zilizotolewa Mwaka 2023-2024. Shughuli na majukumu mbalimbali yamesimamiwa na kutekelezwa kama ifuatavyo: Sekta ya Utawala Ujenzi wa ofisi za Kata Sakina na Osunyai umekamilika bado uwekaji wa samani mpya. Ofisi ya Kata Osunyai wamepatiwa fedha za uwekaji samani Tshs 3,000,000.00 zilizotolewa Mwezi Juni,2023. Ofisi ya Kata ya Moivaro Inaendelea na ujenzi, imepauliwa, kwa sasa inaendelea kupigwa ripu,…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv . Dubai, 25 septemba – Emirates SkyCargo sasa imekuja na suluhisho kwa wateja wake kupitia soko la CargoAi na CargoMART, ikisonga mbele zaidi katika uzoefu wa digital kwa wateja kwa kurahisisha mchakato wa kuagiza mizigo huku mteja akiwa na taarifa halisi za mzigo wake kila hatua. Ushirikiano huu ulianzishwa Uholanzi, Hispania, na Ufaransa, na utawafikia wateja katika nchi zilizochaguliwa barani Ulaya, Amerika, Afrika, Mashariki ya Mbali, na Australasia katika miezi ijayo. Kupitia suluhisho la CargoMART, wateja watapata ratiba za Emirates SkyCargo, viwango vya ushuru na mikataba, pamoja na upatikanaji wa wakati halisi wa mzigo hadi uliopo,…

Read More