Author: Geofrey Stephen

Na Richard Mrusha Geita KAMPUNI ya Nguvu Moja ( Security services ni kampuni ya kizawa asilimia moja na imejipambanua kukupa huduma bora kabisa kwasababu inazingatia vigezo vyote kuanzia wafanyakazi wake wako vizuri kiafya kimorali na ikiakili. Hayo yamebainishwa septemba 23 mwaka huu na Meneja wa Kampuni ya Nguvu Moja Services limited ,Caroline Mushi ambapo amesema kampuni hiyo imekua na tabia ya kuwapima afya wafanyakazi wake kabla ya kuingia kazini, na Mwaka mmoja akiwa kazini. ” Tunapoajiri wafanyakazi wetu, kitu cha kwanza sisi hatutaki mfanyakazi anayeugua ugua kazini, kwahiyo tunampima kabla hajaingia kazini, pia tutampima afya yake baada ya Mwaka mmoja…

Read More

Mwandishi wetu, Arusha Taasisi ya Wanahabari ya kusaidia Jamii za pembezoni (MAIPAC) imeahidi kutoa msaada wa kompyuta kwa shule ya msingi ya Arusha Alliance ambayo inamilikiwa na Walimu ili kuwezesha wanafunzi kusoma masomo ya TEHAMA. Mkurugenzi Mtendaji wa MAIPAC,Mussa Juma alitoa ahadi hiyo katika mahafali ya darasa la Saba ya 14 ya shule hiyo ambapo ni moja kati ya shule 10 bora katika Jiji na Arusha zinazoongoza Kila mwaka mwaka kwa kufaulisha.² Juma ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hiyo alisema kwa shule hiyo ni mfano wa kuigwa nchini kwani imeanzishwa na walimu baada ya kuamua kuungana na kuchangishana fedha…

Read More

Na Gift Thadey, Geita GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Emmanuel Tutubaamewasihi wachimbaji wa madini nchini kutotembea na fedha taslim mifukoni badala yake watumie mifumo ya kielektroniki katika kutoa na kupokea fedha. Gavana Tutuba ameyasema hayo Mjini Geita wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya sita ya kimataifa ya teknolojia ya madini. “Nawashauri wachimbaji kutumia mifumo ya kielelektoniki kupokea na kutoa fedha badala ya kutembea na fedha taslimu,” amesema Tutuba. Gavana Tutuba amesema wao kama BOT wanalipa kwa mfumo wa TIPS ambao unarahisisha kwa kuwa umeunganishwa na mabenki yote na miamala ya simu nchini. “Ndiyo sababu tunawahamasisha…

Read More

Na Richard Mrusha Geita WACHIMBAJI mbalimbali wa madini nchini wameshauliwa kukatia bima mitambo wanayotumia katika shughuli zao za uchimbaji ili pale inapotokea imeharibika ili waweze kutengenezewa bila kuathiri shughuli zao za uchimbaji. Akizungumza katika maonesho ya sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya EPZA Bombambili halimashauri ya mji Geita. Meneja wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) kanda ya ziwa Stella Marwa amesema kuwa bado kumekuwa na muamko wa ukataji bima kwa upande wa wachimbaji ambapo ametoa rai kwa wachimbaji hao kuchangamkia fursa hiyo kutokana umuhimu wa bima hiyo. Aidha ameongeza kuwa katika maonesho hayo pia…

Read More

Na Richard Mrusha Geita MURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Masha Mshomba amesema ,katika kipindi cha uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweza kuongeza thamani ya Mfuko huo kutoka Trilioni 4.8 Hadi kufikia shilingi Trilioni 7.6 kwa hesabu zinazoendelea kukaguliwa Hadi hivi sasa. Mkurugenzi huyo ameyasema hayo mbele ya Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Dkt.Doto Biteko alipotembelea Banda hilo ambapo aliipongeza NSSF kwa hatua hiyo Masha amesema kuongeza thamani ya Mfuko Hadi kufikia kiasi Cha shilingi Trilioni 7.6 ni hatua kubwa ² “Thamani ya Mfuko imeendelea kukua kwa kasi tukizungumzia mahesabu yaliyokaguliwa  hadi mwaka…

Read More

Na Geofrey Stephen A24Tv Uhitimishaji wa namna ya kuwa na Muongozo wa Elimu kwa ajili ya maendeleo endelevu, jambo hili lipo katika Mpango wa nchi za SADC na Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kuwa na Muongozo huo kwa nchi hizo. WAZIRI wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda Ameyasema hayo septemba 22 2023 katika Uzinduzi wa Mpango wa Elimu kwa maendeleo endelevu uliofanyika Jijini Arusha ambapo ameyashukuru mashirika ya Umoja wa Mataifa UNESCO na UNICEF kwa kushirikiana na serikali kuandaa Mpango huo. Alisema nchi za SADC kupitia mawaziri wa Elimu walikutana na kuipa Kazi UNESCO ya kuratibu miongozo hiyo…

Read More

Na Richard Mrusha Geita KAMPUNI ya FEMA MINING AND DRILLING LTD inayojihusisha uchimbaji,ucholongaji na ulipuaji wa madini nchini imeshukuru serikali ya awamu ya sita(6) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Hassan Suluhu kwa kuwapa fursa na nafasi kampuni za kizawa kufanya kazi katika migodi nchini. Akizungumza hayo katika maonesho ya sita ya kitaifa ya teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya EPZA Bombambili Halimashauri ya mji wa mkoani Geita Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea kwenye baada lao Muhandisi Jackline Mtei amesem anapenda kumshukuru Rais DKT. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira wezeshi kwenye…

Read More

Na Richard Mrusha Geita GAVANA wa Benki Kuu (BoT) Emmanuel Tutuba amesema,moja ya majukumu ya Benki hiyo ni pamoja na kushiriki katika masuala ya uchumi ambapo hununua dhahabu kwa ajili ya kutunza akiba za nchi badala ya kutunza kama fedha. Tutuba ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda la BoT kwenye maonesho ya sita ya kitaifa ya teknolojia ya Madini mkoani Geita kwenye viwanja vya EPZA vilivyopo Bombambili halimashauri ya mji wa Geita Amesema lengo la kununua dhahabu na kuziuza nje ya nchi na kupata fedha za kigeni na hivyo kuwezesha kusapoti uchumi wan chi. “Kwa hiyo…

Read More