Author: Geofrey Stephen

Na Mwandishi wa A24tv. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi amewahimiza malezi bora katika jamii ili kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo matumizi ya dawa za kulevya, wizi, ubadhirifu wa mali za umma, udhalilishaji na ulevi. Rais Dk.Mwinyi amesema malezi bora yanaanzia ngazi ya familia, pia amewataka wazazi na walezi Kuwalea vijana katika malezi mema yenye maadili. Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika ibada ya Sala ya Ijumaa Msikiti wa Makuti Kisiwandui Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe :16 Februari 2024. Rais Dk.Mwinyi ameshiriki katika ibada ya sala…

Read More

Na Geofrey Stephen ARUSHA Mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha (IAA)Prof.Eliamani Sedoyeka amemweleza Hayati Edward Ngoyai Lowassa kama kiongozi shupavu aliyeasisi na kusimamia shule za sekondari za kata hapa nchini. Alisema mchango wa Lowassa katika sekta ya elimu ulipelekea ongezeko la shule hizo hapa nchini aliamini elimu ndio kila kitu kwa maendeleo ya taifa lolote duniani huku kipaumbele chake ni elimu, elimu, elimu. “Kabla ya kujenga shule za kata hapa nchini kulikuwa na shule elfu moja tu,baada ya kujenga tulifanikiwa kupata shule 3500 hadi 4000,kwa nchi nzima, ukichanganya na shule za binafsi unapata shule 5000″alisema Sedoyeka Aliongeza kuwa sasa hivi…

Read More

Na mwandishi wetu Dodoma Viongozi na Watendaji wa Wizara ya Madini na Taasisi za Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) na Tume ya Madini leo Februari 15, 2024. wamekutana na ugeni wa Kidplomasia kutoka Ubalozi wa Ufaransa nchini na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti ya Ufaransa (BRGM). Lengo la ugeni huo lilikuwa ni kutambua fursa za uwekezaji hususan kwenye madini muhimu na mkakati na kuangalia maeneo ya ushirikiano katika Sekta ya Madini nchini. Katika kikao hicho kilichongozwa na Naibu Katibu Mkuu Msafari Mbibo, Mtendaji Mkuu wa GST Dkt. Mussa Budeba amebainisha maeneo muhimu ya ushirikiano kuwa ni pamoja na…

Read More

Na Mwandishi wa A24tv. kijana mmoja anayejulikana kwa jina la Larinyoni Saitoti Parmeres (28) mkazi wa kijiji cha Lopuluni kitongoji cha Lopoluni A tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro anatuhumiwa kumuua mke wake Nang’ubukule Ikayo Mbalala (20) kwa kumpiga na rungu na kumkata na kitu chenye ncha kali maeneo mbalimbali ya mwili wake kisha kutokomea kusikojulikana. Akizungumza na maafisa wa shirika la Mimutie linalopambana na kupinga ukatili wa wanawake wilayani Ngorongoro wapofika eneo la tukio mwenyekiti wa kijiji cha Lopoluni Bwn Daniel Kurutut amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jumatano ya Februari 14 2024 ambapo mtuhumiwa baada ya kutenda ukatili…

Read More