Author: Geofrey Stephen

Na WyEST MWANZA Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Profesa Adolf Mkenda amemuagiza Kamishna wa Elimu kufanya uchunguzi wa kina kwa Shule nne zilizobainika kufanya udanganyifu mkubwa katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2022. Prof. Mkenda amesema hayo alipokutana na Wazazi na walezi wa Wanafunzi waliofutiwa matokeo ya Mtihani wa Kidato nne 2022 wa Shule ya Sekondari Thaqaafa ya Jijini Mwanza kwa ajili ya kuwasikiliza. Amezitaja shule hizo kuwa ni Cornelius ya Kinondoni Dar es Salaam, Thaqaafa ya Mwanza, Mnemonic ya Zanzibar na Twibhoki iliyoko Mara na kumtaka Kamishna huyo kuchukua hatua kali kulingana na ripoti ya uchunguzi…

Read More

Na Richard Mrusha kigoma Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa amesisitiza kuwa, Serikali inawathamini wazalishaji wa Chumvi hapa nchini ili kuongeza uzalishaji wa chumvi kwa kuhakikisha kuwa inaondoa changamoto zote zinazokwamisha maendeleo katika Sekta ya Madini kuwawezesha wachimbaji wa madini wafanye shughuli za uchimbaji madini kwa tija. Dkt. Kiruswa ameyasema hayo Februari 18, 2023 alipotembelea eneo la machimbo ya chumvi la Chakulu wilayani Uvinza mkoa wa Kigoma ili kuzungumza na kikundi cha Kinyo Farmers and Salt Works na Kikundi cha Twikome Salt Kinyo Chakulu. “Ninasisitiza kuondoa migogoro katika eneo hili ili kuchochea ongezeko la uzalishaji wa Chumvi hapa…

Read More

Menejimenti ya Tume ya Ushindani nchini ( FCC) ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bw. William Erio, imetembelea Bandari ya Tanga kwa lengo la kujionea utendaji wake huku ikiahidi kutoa ushirikiano wa kutosha katika kukabiliana na suala la uingizaji wa bidhaa bandia. Akizungumza wakati wa ziara hiyo akiwa Bandarini hapo, Bw. Erio pamoja na kupongeza jitihada zinazofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika katika kutekeleza miradi mikubwa itakayoinua, kukuza uchumi wa Nchi na kuleta maendeleo kwa watanzania ikiwa ni pamoja na upanuzi wa bandari ya Tanga unaoendelea kufanyika sasa, alisisitiza kuwa FCC kulingana na utekelezaji wa majukumu…

Read More

Na WyEST, BUTIAMA – MARA Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda amekitaka Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT) kilichopo Butiama mkoani Mara kujikita kutoa mafunzo kwenye eneo la kilimo kwa upana wake ambao ndio msingi halisi wa uanzishwaji wa chuo hicho. Prof. Mkenda ameyasema hayo Wilayani Butiama alipotembelea chuo hicho na kuwataka kuhakikisha kuwa pamoja na mafunzo wanafanya tafiti na kusambaza matokeo ya tafiti hizo ili kunuifaisha wakulima kwa kuongeza tija na uzalishaji. Waziri Mkenda ameeleza kuwa chuo hicho kitaanza rasmi kutoa mafunzo mwaka huu 2023 na kuagiza uongozi wa…

Read More

Na Doreen Aloyce, Dodoma Kufuatia kuwepo kwa vitendo vya ulanguzi usio halali wa mazao kwa wakulima hapa nchini Bodi ya usimamizi wa Stakabadhi Za Ghala (WRRB) imetoa wito kwa walanguzi wa mazao kuacha kuwalagai wakulima kwa lengo la kujinufaisha. Kauli hiyo imetolewa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Bodi hiyo Asangye Bangu Wakati akielezea utekelezaji wa bodi hiyo kwa waandishi wa habari ambapo amesema hali hiyo imeifanya Serikali kuchukua hatua ya kuanzisha mfumo ambao utasaidia kuondoa hali ya sintofahamu kwa wakulima. Ambapo Bangu amesema kuwa kumekuwa na wimbi la watu wanakwenda mashambani kwa wakulima na kuwadalalia mazao na kununua kwa bei…

Read More

Na Mwandishi wa A24Tv Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.)amekishauri Kiwanda cha Kioo Limited kuendelea kuzalisha bidhaa za kioo kwa wingi na zenye ubora na viwango vinavyohitajika kwa ajili ya Soko la Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA). Aidha, amekishauri Kiwanda hicho kuzalisha bidhaa za kioo zitakazotumika kama vifungashio kwa ajili ya wajasiliamali wadogo wadogo ili waweze kuhimili ushindani katika biashara na kuweza kuingia katika soko la AfCFTA. Dkt. Kijaji ameyasema hayo alipotembelea Kiwanda cha Kioo Limied kilichopo Chang’ombe, jijini Dar es Salaam 14/02/2025 kwa lengo ya kuangalia bidhaa za kioo zinazozalishwa na kiwanda…

Read More